Menu

Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. 2 Huyo mwanzo

Tuesday, October 28, 2014

NGUVU YA MUNGU ILIYOPO KATIKA KINYWA CHAKO.

NGUVU YA MUNGU ILIYOPO KATIKA KINYWA CHAKO.



BWANA YESU asifiwe Wana wa MUNGU.

Napenda kuleta kwenu somo hili:

                        Je Unakiri nini?


 “Nanyi mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu ROHO MTAKATIFU, (Matendo 1: 8).

Je, tunatumia hii nguvu ya MUNGU?

Na je tunaitumia  mamlaka ya KRISTO tuliyopewa kama inavyotakiwa?

Haijalishi mwana wa MUNGU unapita katika magumu kiasi gani, Unachotakiwa ni kubadilisha kukiri kwako, na kadri unavyotamka kinyume na mazingira yanavyoonekana,elewa kuna jambo katika ulimwengu wa Roho linafanyika, hata kama huna shilingi mia mfukoni wewe sema pesa zipo,  hata kama wewe ni mgonjwa umelala kitandani Sema mimi ni mzima, maana Neno la MUNGU  linasema aliye dhaifu na aseme ana nguvu.

 Ezekieli alipoonyeshwa lile bonde la mifupa mikavu, kwa macho  ya damu na nyama aliona haiwezekani kwa ile mifupa mikavu kuwa na uhai tena ,lakini MUNGU akamwambia itabirie hii mifupa mikavu ipate kuishi.

Ndipo Ezekieli akatambua nguvu iliyopo katika kinywa chake, akaanza kutoa unabii na kuitabiria ile mifupa, akaiambia  ’’ enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la BWANA; BWANA MUNGU aiambia mifupa hii maneno haya; Tazama nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi .Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na kuwafunika ngozi, nakutia pumzi ndani yenu nanyi mtaishi.’’  Maneno haya tunayapata katika kitabu cha (Ezekieli 37:1…..)

Katika maandiko haya tumeona, ni jinsi gani Ezekiel ialivyoweza kutumia nguvu na uweza ulioko ndani ya kinywa chake na kuweza kuleta uhai tena. Na wewe mwana wa MUNGU nini ni kimekuwa mifupa mikavu katika maisha yako?

-Yamkini ni ndoa ndio imekuwa mifupa mikavu itabirie nayo itakuwa hai tena,

-au ni uchumi wako,

- afya yako,

-watoto wako,

-hudumayako,

MUNGU anakuambia leo simama na uvitabirie, maana kuna nguvu katika kutamka.



Unakiri nini kushindwa au kushinda?

Nguvu ya MUNGU iko juu yako, badilisha yale yote yanayoonekana kuwa yameshindikana na yatawezekana kupitia kinywa chako katika Jina la YESU KRISTO mwenye nguvu zote. AMEEEN.

MUNGU awabariki sana. 

Thursday, October 23, 2014

USIYAONE MATATIZO YA KIUCHUMI KAMA KIKWAZO - MWALIMU MWAKASEGE






mwakasege

Shalom,

Tunajua unataka uwe na uchumi mzuri. Hii ni kwa mwanadamu yeyote bila kujali mahali alipo,awe anafanya kazi au hata kama hafanyi kazi.

Kuanzia leo na siku kadhaa zitakazofuata,tutajitahidi kukushirikisha misingi kadhaa iliyomo katika biblia,ambayo tunaamini itakusaidia uwe na uchumi mzuri. Msingi wa kwanza ni huu:Badilika unavyoamini juu ya uchumi,utabadilika unvyosema juu ya uchumi,na hali yako ya uchumi itabadilika vivyo hivyo.

Tunaamini ya kuwa; mtu akibadilika anavyoamini atabadilika pia anavyosema;na hali yake ya maisha itabadilika vivyo hivyo.
Jambo hili tunalipata tunaposoma kitabu cha Mithali 23:7 ya kuwa; “Maana aonavyo nafsini mwake,ndivyo alivyo.”
Tafsiri nyingine ya mstari huu inasema;”maana awazavyo nafsini mwake ndivyo alivyo.” Tasfiri nyingine ya mstari huu inasema;”maana aaminivyo nafsini mwake,ndivyo alivyo.” Mstari huu unataka tujue ya kuwa maisha ya mtu alivyo ni matokeo ya awazavyo au aaminivyo au afikirivyo(mindset), nafsini mwake.

Ulivyo kimaisha kwa nje ni matokeo ya msimamo wako wa kimawazo ndani yako. Kwa ulivyo kiuchumi,ni matokeo ya msimamo wako kimawazo(mindset),ulionao ndani yako juu ya uchumi.

Wapelelezi 10 walileta habari mbaya walipotoka kuipeleleza Kaanani,kwa vile waliamini mioyoni mwao ya kuwa “majitu” waliyoyakuta Kaanani yalikuwa kikwazo na pingamizi kwao.Wapelelezi wawili (Yoshua na Kalebu),waliona hayo “majitu” pia lakini mioyoni mwao waliamini tofauti. hawakuyaona majitu kama kikwazo bali waliyaona kama fursa kwao ya kutatua tatizo hilo ili waweze kula.

Soma habari hii katika kitabu cha hesabu 13:32,33 na Hesabu 14:9,28
Matokeo ya tofauti hizo kuwaza na kuamini,kuliamua hatma ya baadaye ya uchumi na maisha yao.Wapelelezi 10 waliishia kulalamika na kushindwa kwenda Kaanani. Na wale wawili (Yoshua na Kalebu) waliweza kwenda Kaanani na wakawa na maisha mazuri.

Wazo tunalokufikirisha siku hii ya leo ni kwamba;Usiyaone matatizo ya kiuchumi yanayokuzunguka kama kikwazo,bali yaone fursa ya kuyatatua ili iwe njia mojawapo ya kuongeza kipato chako. Kumbuka wanaolalamika wanapoona matatizo,wanajipofusha fikra szao wasiona fursa za kimaendeleo katika matatizo hayo.

Mungu awabariki.

Saturday, October 18, 2014

NINAWEZAJE KUSHINDA DHAMBI KATIKA MAISHA YANGU YA UKRISTO?

Ninawezaje kushinda dhambi katika maisha yangu ya kikristo?

Swali: "Ninawezaje kushinda dhambi katika maisha yangu ya kikristo?"

Jibu: Biblia inazungumzia juu ya vitu hivi tulivyonavyo ili tushinde maisha yetu ya dhambi:

(1) Roho Mtakatifu – kipawa kimojachapo ambacho Mungu ametupa (kanisa lake) kwa ajili ya kuwa na ushindi katika maisha ya kikristo ndani ya Roho Mtakatifu. Mungu anatofautisha mtendo ya mwili na matunda ya Roho Mtakatifu katika wagalatia 5:16-25. katika andiko hilo tunashauriwa kutembea katika uwepo wa Roho Mtakatifu. “waumini wote tayari wamejazwa na Roho Mtakatifu”,lakini hapa tunasisitizwa kupatia nafasi Roho Mtakatifu atutawale na kutuongoza. Hii ina maana ya kuwa tusikilize sauti yake tusije tukatenda mapenzi yetu wenyewe.

Tofauti ambayo Roho Mtakatifu anaweza kuifanya maishani mwa mtu ni kama ile ya Petro, kabla hajajazwa Roho Mtakatifu alimkana Yesu mara tatu, na alikuwa mbeleni ameahidi kumfuata Yesu mpaka kwenye hatari ya kifo angekufa naye. Baada ya kujazwa na Roho alizungumza waziwazi na kwa ujasiri mbele ya wayahudi juu ya mwokozi katika siku ya pentekote.

Unatembea ndani ya Roho ukiwa humzuii anapotaka kujidhihirisha (“kumzima Roho” wathesalonike wa kwanza 5:19) na una kiu ya kujazwa naye kila wakati (Waefeso 5:18-21). Je mtu hujazwaje na Roho Mtakatifu? Kwanza ni kwa mapenzi ya Mungu kama vile ilivyo katika agano la kale. Alikuwa akichagua watu Fulani, kuwajaza kwa ajili ya kutekeleza kazi ama wadhifa Fulani (Mwanzo 41: 38; Kutoka 31:3; Hesabu 24:2; Samueli wa kwanza 10:10; na kadhalika.) Ninaamini kuwa kuna ushahidi katika Waefeso 5:18-21 na Wakolosai 3:16 yakuwa Mungu huchagua kujaza wale wanaojijaza Neno la Mungu kwa kuwa kote kote ni kujazwa uwezo wa Mungu.

(2) Neno la Mungu, Biblia – Timotheo wa pili 3:16-17 inasema ya kwamba Mungu ametupa neno lake ili lituandae katika kufanya kazi njema. Linatufundisha jinsi ya kuishi na cha kuamini, linatufunulia kama tumetenda makosa na kuturudisha katika njia ya sawa. Kama waebrania 4:12 inavyosema Neno la Mungu liko hai na lina nguvu ya kupenya ndani ya nafsi zetu kung’oa lile tatizo ambalo mwanadamu hangeweza kulitatua. Mwandishi wa zaburi azungumzia uwezo wa Neno la Mungu juu ya kubadilisha maisha ya watu katika zaburi 119:9,11,105 na aya nyengine. Joshua aliambiwa siri ya kushinda adui zake (inayoashiria pia vita vyetu vya kiroho) ni kwamba asilisahau Neno la Mungu bali alitafakari usiku na mchana ili akalitimize. Haya aliyatenda, ijapokuwa maagizo yenyewe hayakuwa na uhusiano na mambo ya kivita lakini yakampa ushindi katika vita vya kuimiliki nchi ya ahadi.

Hii ni sehemu ambayo mara nyingi tunaipuuza. Tunapenda kubeba biblia tukienda kanisani ama kusoma aya za kukariri lakini hatuyatilii maanani yale tuyasomayo. Hatuyatafutii nafasi maishani mwetu kiasi cha kutubu dhambi zetu na kumtukuza Mungu kwa kipawa hiki. Tunasoma tu kiasi cha kupata mtazamo Fulani juu ya wokovu lakini hatuongezi juhudi zozote katika kutafakari kwetu mara kwa mara kiasi cha kutufanya tuwe na afya nzuri kiroho.

Ni muhimu sana kwako ufanye tabia ya kusoma neno la Mungu. Kama bado hujazoea basi Roho anakusisitiza uwe na tabia ya kulisoma Neno la Mungu. Nina kushauri uwe na kumbukumbu ya yale uliyoyasoma kwa kuyanakili kwenye daftari lako au kwenye kompyuta. Biblia ndicho kifaa Roho hutumia katika maisha yetu na maisha yaw engine (Waefeso 6:17), ikiwa ni sehemu kubwa ya silaha mojawapo ambayo Mungu hutupa ili tupigane vita vya kiroho (Waefeso 6:12-18)!

(3) Maombi – Hii pia ni njia nyengine ambayo Mungu ametupatia. Njia hii wakristo wengi huitaja tu kwa maneno lakini hawaitumii. Tuna ibada za maombi na nyakati za maombi na kadhalika lakini hatuoni manufaa ya jambo hilo sawa na kanisa la kwanza (Matendo 3:1; 4:31; 6:4; 13:1-3, na kadhalika). Paulo mara kwa mara arudia kueleza vile alikuwa akiwaombea wale aliokuwa akiwahudumia. Lakini tunapokuwa peke yetu hatuitumii njiaa hii. Mungu ametuahidi mambo mazuri ya ajabu kuhusiana na maombi (Mathayo 7:7-11; Luka 18:1-8; Yohana 6:23-27; Yohana wa kwanza 5:14-15, na kadhalika.) Paulo analiongezea mkazo tena katika mafundisho yake juu ya kujiandaa kwa ajili ya vita vya kiroho (Waefeso 6:18)!

Je, ni muhimu kiasi gani njia hii? Tunapomtazama tena Petro, tunaona maneno ya kristo aliyomwambia kabla hajamkana kule Gethsemane. Yesu alipokuwa akiomba Petro alilala. Yesu akamwambia, “Kesheni mkiomba ili msiingie majaribuni: Roho inataka lakini mwili ni dhaifu” (Mathayo 26:41). Wewe pia kama Petro unataka kufanya mema lakini huna nguvu yakutosha kufanyia hayo. Lazima tufuate mausia ya Mungu, tuendelee kumtafuta, tukibisha na kumuuliza… na atatupatia nguvu ile tuitafutayo (Mathayo 7:7 na kuendelea). Lakini lazima tuitilie mkazo njia hii maishani mwetu ndiyo tufaulu. Sisemi ya kwamba maombi ndiyo njia maalum zaidi. La sivyo. Mungu ni wakutisha. Maombi ni kukubali hali zetu za udhaifu, ukuu wa Mungu mwenye nguvu na asiyeshindwa ili tupate uwezo huo huo tuweze kuyafanya yaliyo mapenzi yake (wala si yetu) (Yohana wa kwanza 5:14-15).

(4) Kanisa – Hii ni mojawapo ya njia tunazozifumbia jicho. Yesu alipowatuma wanafunzi wake aliwatuma wawili wawili (Mathayo 10:1). Tunaposoma juu ya habari za safari za wale wamishenari katika kitabu cha matendo ya mitume, hawakuenda mmoja mmoja bali katika makundi, wawili wawili au zaidi.Yesu alisema mahali wawili au watatu wamekusanyika kwa ajili ya jina langu, nami nitakuwa katikati yao (Mathayo 18:20). Anatuamuru tusiache kukusanyana pamoja kama kawaida za watu wengine zilivyo bali tuutumie wakati wa kuwa pamoja kwetu kwa kutiana moyo katika upendo na matendo mema (Waebrania 110:24-25). Anatuagiza kutubu dhambi zetu mmoja kwa mwingine (Yakobo 5:16). Katika habari za hekima katika agano la kale tunaambiwa ya kwamba chuma hunoa chuma mwenziwe, vivyo hivyo mtu huchangamsha sura ya rafiki yake (Methali 27:17) “kamba ya nyuzi tatu haikatiki rahisi.” “kuna nguvu katika umoja wa wengi (Mhubiri 4:11-12).

Baadhi ya watu ninaowafahamu wamepata kaka na dada katika kristo wanaotangamana pamoja au kwa simu na wanaelezana vile wanaendelea na maisha ndani ya kristo na wanawajibika katika kuombeana huku wakiishi maisha sawa na Neno la Mungu. Mabadiliko mara nyingine huja haraka na wakati mwengine polepole. Lakini Mungu ametuahidi ya kwamba kadri tunavyoendelea kutumia njia hizi alizotuwekea, ndivyo atatuletea mabadiliko maishani mwetu. Vumilia ukijua ya kuwa ni mwaminifu katika ahadi zake.

KANUNI ZA KUISHI MAISHA YA USHINDI NA BARAKA TELE SOMA HII



   Kila jambo analokutana nalo mwanadamu lina sababu ya kuwepo, na kuna nguvu inayolishikilia hilo jambo liendelee kuwepo. Endapo hiyo nguvu itakatwa, basi hilo jambo haliwezi kuendelea kuwepo. Na uwepo wa nguvu unaosababisha mambo kutendeka unategemea kanuni; ili usipate magonjwa ya kuambukiza, zipo kanuni za kujiepusha na magonjwa hayo.

   Na katika mambo ya rohoni, kuna kanuni za kuyapata hayo mambo ya rohoni; ili ubarikiwe, ule matunda ya kazi za mikono yako na upokee uponyaji ni lazima uzingatie kanuni. Na kanuni hizo ni; uwe mnyenyekevu kwa Mungu, na unyenyekevu huo uambatane na maombi, maombi yaliyokusudia kuutafuta na kuuona uso wa Mungu, na ili uweze kuuona uso wa Mungu ni lazima uachane na njia zote mbaya.

2 Nyakati 17:13-14 “Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao”.

   Hapa neno mvua linabeba maana mbili; mvua kwa maana ya mvua, na mvua kama baraka. Na katika baadhi ya vitabu vitakatifu vya Biblia, Mungu analithibitisha hilo; (Isaya 30:23 Naye atatoa mvua juu ya mbegu zako, upate kuipanda nchi hii; na mkate wa mazao ya nchi, nayo itasitawi na kuzaa tele; katika siku hiyo ng’ombe zako watakula katika malisho mapana), mvua kama baraka- Malaki 3:10 “. . . mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la”.

Kwa hiyo, mbingu zikifungwa kusiwe na mvua; mvua kama mvua inaweza isinyeshe na mvua kama baraka inaweza pia isipatikane. Na ukikosa baraka, basi una laana; inaweza ikawa ni laana ya ukoo, laana ya kutamkiwa (Mithali 11:26, 24:24,) au ya kujitamkia kwa kujua au pasipo kujua, au laana inayotokana na kutenda dhambi (Kumbukumbu la torati 28:15, Malaki 2:2, Zaburi 119:21).

   Nzige kula nchi; nzige hula mimea au mazao yaliyootayo juu ya nchi, wanapokula mazao hula chakula cha binadamu (Zaburi 105:34-35 “Alisema, kukaja nzige na tunutu wasiohesabika wakaila miche yote ya nchi yao, wakayala matunda ya ardhi yao”). 

Unaweza kuwa na huduma iliyodumaa au imekufa kabisa, unafanya kazi lakini huli matunda stahili ya kazi yako au wewe ni mkulima lakini mavuno ni hafifu. Katika hali hizo, nzige wamekula nchi, ni lazima ufanye jambo kuikomboa nchi hiyo; kuinua au kufufua huduma yako, kunufaika na kazi ya mikono yako na hata kupata mavuno bora ya mashamba yako. Jambo hili linaweza kusababishwa na nguvu  za ufalme wa giza au maisha ya dhambi (Zaburi 119:21), lakini unaweza kujikomboa katika utumwa huo, zingatia kanuni.

   Tauni; neno hili linawakilisha magonjwa, ambayo yanaweza hata kuondoa uhai au kukuacha na ulemavu. Magonjwa yasiyo na tiba au magonjwa yasiyoeleweka yanasababishwa na nini, na inaweza ikawa ni malipo ya dhambi (Ayubu 8:3-4, 2 Samweli 24:15) au ni kuonewa na shetani. Lakini hayo yote yanaweza kukuachilia huru tangu sasa, ikiwa yamekupata wewe au ndugu yako, Mungu ni mwaminifu hakuwahi kusema uongo hata leo asema uongo.

Katika mambo hayo matatu; kukosa mvua, nzige kula nchi na tauni, inawezekana ukawa umepitia jambo moja wapo au yote kwa jinsi tulivyoyaona maana zake katika mwaka huu (2012) unaomalizika hivi karibuni. Na hungependa kuingia na kutembea na mwaka unaofuata (2013) na mambo hayo, unatamani kufunguliwa na kuwekwa huru; upokee baraka kutoka kwa Mungu, kuinua na kufufua huduma yako, kula matunda ya kazi za mikono yako na kuishi maisha yasiyojua ugonjwa/magonjwa, INAWEZEKANA! Zipo kanuni alizoziweka Mungu mwenyewe ili tupone, zingatia kanuni hizo. Kanuni hizo ni:-

   Kunyenyekea; ni kutii na kukubali sauti ya Mungu na kufanya yanayoelekezwa na sauti hiyo (Isaya 1:19 “. . . mkikubali na kutii, mtakula mema ya nchi”). Sauti ya Mungu siku zote inatuelekeza kuifuata njia njema, na kuifuata njia njema ni kuchagua mema; baraka, uponyaji, ushindi, heshima, kuinuliwa na mengine mengi mazuri. Kunyenyekea kunamfanya Mungu atumie muda wa ziada kututegea sikio na kuyasikiliza maombi yetu, na Mungu akiyasikiliza maombi yetu lazima tuwe na uhakika wa kupokea majibu (Danieli 12:10, Isaya 66:2). 

Kutonyenyekea kunainua hasira ya Mungu juu ya wanadamu, na ndipo tunapatwa na mabaya (Yeremia 44:10). Kwa hiyo hii ni kanuni ya kwanza, ukitaka kuwa rafiki wa Mungu na kupokea mema kutoka kwake, lazima unyenyekee.

   Kuomba; ni njia ya mwanadamu kuzungumza na Mungu (Isaya 1:18 “. . . haya njooni tusemezane. . .”), Mungu anaposema ‘njooni tusemezane’ anatufundisha kuomba ili tupeleke mahitaji yetu kwake na yeye atujibu kulingana natulivyoomba au tunavyostahili (Yakobo 5:13). 

Kuomba ni kanuni ya pili, ambayo ni lazima iambatane na kanuni ya kwanza (unyenyekevu), huwezi kuwa muombaji kama hunyenyekei. Unyenyekevu unakupa haki mbele za Mungu, na maombi ya mwenye haki ndiyo yanayofaa sana (Yakobo 5:16 kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii). Na hii ni kanuni ya pili.

   Kuutafuta uso wa Mungu; kama tulivyoona, hizi kanuni zina mfuatano wa kutegemeana, unapokuwa mnyenyekevu na muombaji ni rahisi sana kukutana na Mungu. Unapoomba hakikisha umekutana (umekuwa-connected) na Mungu na ndipo ueleze mahitaji yako. Jambo hili si jepesi, unahitaji kujitoa na kudhamiria; kuwa mnyenyekevu na muombaji na ndipo utakapokutana na Mungu (Mithali 8:17 . . . na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. Yeremia 29:13 . . .nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote). Kanuni ya tatu.

Kuacha njia mbaya; ni kurudi kutoka dhambini na kumrejea Mungu. Unyenyekevu, maombi na kuutafuta uso wa Mungu ni lazima viambatane na toba, kila unaposogea mbele za Mungu hakikisha unajitakasa hata kama hukumbuki kumtenda Mungu dhambi (Hosea 5:15 . . . hata watakapoungama makosa yao na kunitafuta uso wangu. . .). Ukiamua kuacha njia mbaya, usijiweke tena katika mazingira ya kuirudia hiyo njia mbaya; epukana na mazingira ya kutenda dhambi kwa kuangalia, kusikiliza au kuongea (Yeremia 36:7 na kurudi, kila mtu akiiacha njia yake mbaya. Yeremia 35:15 rudini sasa, kila mtu na aiache njia yake mbaya, mkatengeneze matendo yenu). Na siyo utende dhambi makusudi kwa kuwa utaomba toba!! Kanuni ya nne.

Ni wewe mwenyewe, unayeweza kuamua na kujitoa kutoka katika maisha ya mateso na kuonewa na yule mwovu. Zingatia kufuata, kutenda na kuzitimiza kanuni, amua leo kuingia mwaka mpya na maisha mapya. Mungu akubariki sana, kwa jina la Yesu Kristo.

UMEJIANDAA KUSAIDIA WAAMINI WAPYA?, MAISHA YA USHINDI KATIKA KRISTO YESU



Pengine unajiuliza. ‘Nani? Mimi? Sijui la kusema; sijawahi kusoma shule ya Biblia; hakuna mtu amewahi kunifundisha jinsi ya kufanya hivyo’. Kumbuka Yesu aliwatumia watu wa kawaida wasio na elimu ya shuleni. Mdo 4:13 ‘Basi walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na kuwajua ya kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa, wakastaajabu, wakawatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu’.

Hatuhitaji kuwa wakamilifu ndipo tuanze kazi hii. Mungu alimuahidi Musa, ‘Nitakuwa pamoja nawe’ (Kut 3:12). Na Yesu aliwaahidi wanafunzi wake, ‘mimi nipo pamoja nanyi sikuzote, hata ukamilifu wa dahari’ (Mt 28:20). Wanafunzi wake hawakuwa shujaa sana ndiyo maana walikimbia Yesu alipokamatwa katika bustani ya Getsemane. Lakini walipojifunza kwamba Yesu yuko pamoja nao, wakawa tayari kufanya lolote alilowataka wafanye.
Mungu ndiye anayetupa uwezo, hekima na ujasiri ili tumalize vyema.1 The 5:24 Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya’.

Hata hivyo, kuna mambo kadhaa yanayopaswa kuonekana katika maisha yetu kama tunataka kusaidia wengine wakue katika maisha yao ya Kikristo.

1)   Tuwe na maisha ya ushindi katika majaribu na dhambi (1 Pet 2:12). Tutaishi maisha ya ushindi tukiwa na uhusiano wa upendo na ushirika na Yesu Kristo na tukiwa tumejazwa Roho Mtakatifu.
2)   Tuwe tayari kujitoa kwa ajili ya mwingine anayetaka kukua. Uanafunzi unahitaji muda. Wanafunzi wajue kwamba wanaweza kutujia wakati wowote wanapotaka kutushirikisha mawazo yao na matatizo yao.
3)   Tujue kwamba tunatakiwa kutunza siri za yale wanayotuambia bila kuyasema kwa wengine. Wanahitaji kujua kwamba hata kama watatushirikisha ugumu wowote au dhambi ya siri, hatutawahukumu. Wanahitaji kujua kwamba wana thamani kwetu.
4)   Tuwe tayari kuomba msamaha tunapowakosea. Wanahitaji kujua kwamba hatujafikia ukamilifu lakini tunapitia magumu wanayoyapitia.
5)   Tuwe jasiri kusema ukweli ili kuwakemea na kuwaonya wanafunzi wetu wakiendelea na mwenendo mbaya (Lk 17:3). Lakini wakati wote tujitahidi kuongea katika upendo (Mit 17:17a).
6)   Tuwe tayari kuacha kufanya jambo ambalo tunaona kwamba linamsababisha mwanafunzi ajikwae (Rum 14:1-3, 13-15, 19-21).

Mambo muhimu ya kukumbuka kuhusu uanafunzi:
1)   Ni Mungu anayefanya kazi ya kuwabadilisha wanafunzi. Roho Mtakatifu analitumia Neno la Mungu kuwabadilisha watu. (Fil 2:13; 1 Kor 3:6).
2)   Tusiwe wakubwa sana kwa wanafunzi wetu. Badala yake tuwe watumishi wa kiroho. Wajifunze kufanya analotaka Mungu na sio tunanalotaka sisi wala wanalotaka wao. Kol 1:28.
3)   Tunaweza kutoa mafunzo kwa maneno yetu, lakini mfano wa kuigwa ni muhimu pia.
4)   Kumsaidia mwingine akue kunahitaji uhusiano. Mwalimu asijione kwamba ni muhimu kuliko mwanafunzi wake.
5)   Uanafunzi ni urafiki, kwanza na Mungu na kisha na waamini wengine.

III. MOYO WA ‘MFANYA UANAFUNZI’
1)   Moyo wa maombi
1 The 1:2-3 Paulo aliombea wengine.
Yn 17 Yesu aliombea wanafunzi wake, na sisi tumejumuishwa.
Kol 4:12 Epafra aliwaombea kwa bidii.
Hebu angalia Paulo alivyoombea: Efe 1:15-18; Fil 1:3-11; Kol 1:3-14.
2)   Moyo wa ushujaa
1 The 2:2 Paulo hakusubiri waamini wapya wamjie kwa ajili ya kuomba msaada. Aliwaendea ingawa alipata mateso mengi huko Filipi.
3)   Moyo wa mama
1 The 2:7  Waamini wapya wanahitaji upole na huruma. Yaani, tuwasikilize vizuri kabla ya kuongea na tuonyeshe upendo badala ya hukumu.
4)   Moyo wa baba
1 The 2:11-12 Wakati mwingine tunatakiwa kuwafundisha mambo magumu ili wajifunze kuwa jasiri na kusimama katika imani yao. Tuwafundishe kujitegemea. Wakati mwingine tuweke wazi udhaifu wao na dhambi zao.
5)   Moyo wa kushirikisha nafsi
1 The 2:8  Waamini wapya wanahitaji mambo mengine zaidi ya mafunzo peke yake. Tunatakiwa tushirikishe maisha yetu yote kwao. Mfano:
 a) Kuwa tayari kuwashirikisha magumu tunayopitia bila kusahau ushindi
     tunaoupata.
b) Fanya matembezi nao. Nendeni dukani pamoja, kuchota maji na hata
     kutembelea wagonjwa.
c) Wakaribishe nyumbani kwako. Wanahitaji kuona jinsi tunavyoishi. Wanahitajikuona kwamba si kila kitu ni kamili katika nyumba zetu. Wanahitaji kuona tunavyohusiana na wenzi au watoto wetu. Wanahitaji kuona tunaadibisha vipi watoto wetu.
6)   Moyo usio na lawama.
1 The 2:10 Tukumbuke kwamba tunayotenda yana sauti zaidi kuliko tunayosema. 1 The 2:3-6.

IV.UTEKELEZAJI
1.Jiandae vizuri. Msikilize Roho akuongoze kwamba uanze na somo gani.
2.Uwe na lengo kichwani kwa ajili ya mwanafunzi wako.
3.Uwe na maandiko ya kutumia. Usitumie maandiko mengi sana kwa wakati mmoja.
4.Uwe na mifano hai ya kuelezea unachofundisha.
5.Uwe na andiko la kukumbuka. Likariri pamoja naye ili aone kwamba hata wewe unapenda kuliweka Neno moyoni mwako.


USHAURI
Ndugu msomaji/mwanafunzi, napenda kukutia moyo kwa utayari wako wa kujifunza masomo haya ya kufanyika mwanafunzi wa Yesu. Mpango wa Mungu kwako si kuwa mshirika wa kanisa tu, bali kuwa mwanafunzi wa Yesu (Mt 28:19) Jitahidi kumaliza masomo yote (kozi nzima) ya uanafunzi ili ufae kufundisha na wengine (2 Tim 2:2).



Dr Lawi E. Mshana, Founder & President
Victorious Life Ministries

Box 554 Korogwe, Tanga, Tanzania.

Alhamisi, 26 Juni 2014


UANAFUNZI - Somo linaendelea

3. Mwanafunzi lazima:-
a)   Ajifunze kwa mwalimu wake (head knowledge). Ni muhimu mwanafunzi kuwa na mwalimu wa kumpa mafundisho ya kiroho badala ya kutegemea mafundisho ya kidini.
b)   Apende mafundisho (heart knowledge). Hapa anakubali kwamba haya mafundisho ni kwa ajili yake. Hatafuti kujifunza kwa ajili ya watu wengine.
c)    Atendee kazi (applied knowledge). Hapa mafundisho yanakuwa sehemu ya maisha yake. Anayatumia kuleta mabadiliko maishani mwake.
d)   Ashirikishe (transferred knowledge).  Hapa anayashirikisha kwa wengine
      2 Tim 2:2. Hapa ndipo anafikia hatua ya kuyashirikisha kwa wengine kwa vile
      yamembadilisha yeye mwenyewe tayari.

4. Petro, Barnaba na Paulo

Petro hakuwa na elimu ya kidunia isipokuwa alijifunza kwa Yesu na akawahubiri maelfu wakaokoka. Mdo 2:40, 41 ‘Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu’.

Ni Barnaba aliyemlea Paulo. Mdo 9:26-27 Na Sauli alipofika Yerusalemu, alijaribu kujiunga na wanafunzi, nao walikuwa wakimwogopa wote, wasisadiki ya kuwa yeye ni mwanafunzi. Lakini Barnaba akamtwaa, akampeleka kwa mitume, akawaeleza jinsi alivyomwona Bwana njiani, na ya kwamba alisema naye, na jinsi alivyohubiri kwa ushujaa katika Dameski kwa jina la Yesu’. Walisafiri pamoja katika huduma (Mdo 11:25-26) mpaka walipopishana kwa ajili ya Yohana Marko aliyewaacha katika safari za kimisheni (Mdo 15:36-40). Barnaba alichagua kumchukua Yohana Marko kwa ajili ya kumfanyia uanafunzi zaidi. Baadaye akafaa zaidi hata kwa Paulo. Kol 4:10 Aristarko, aliyefungwa pamoja nami, awasalimu; na Marko, mjomba wake Barnaba, ambaye mmepokea maagizo kwa habari yake; akifika kwenu mkaribisheni’.
Paulo alimfanyia uanafunzi Timotheo ili aiendeleze huduma pale aliposhindwa kuendelea mwenyewe. 1 Tim 1:2,3 kwa Timotheo, mwanangu hasa katika imani. Neema na iwe kwako, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu. Kama vile nilivyokusihi ukae Efeso, nilipokuwa nikisafiri kwenda Makedonia, ili uwakataze wengine wasifundishe elimu nyingine’.

5.Wakristo waliokomaa wanafananaje?

Efe 4:13 ‘ – hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo’. Hili ndilo lengo letu. Lakini kivitendo ina maana gani?

a)   Wako salama katika uhusiano wao na Kristo. 1 Yoh 5:11-13 Wanajua wana uzima wa milele.
b)   Wanatambua mamlaka ya Bwana Yesu maishani mwao. Kol 2:6-7; 1 Kor 8:6.
c)    Wana ushindi katika dhambi maishani mwao. 1 Yoh 5:4-5; 1 Kor 10-13.
d)   Wanayajua maandiko na wanaweza kuyatumia inavyotakiwa katika maisha yao. 2 Tim 3:16-17
e)   Wana maisha ya maombi yenye matokeo. Fil 4:6-7; 1 The 5:16-18.
f)    Tunda la Roho linaonekana maishani mwao. Gal 5:22-23; Yn 15:8.
g)   Wana utii katika kumtumikia Bwana. Yn 14:15,23; 1 Yoh 2:3.
h)   Wanashirikisha kikamilifu imani yao kwa wengine. 1 Pet 3:15.
i)     Wanashiriki kikamilifu katika ushirika wa Kikristo (ibada). Ebr 10:24-25.
j)    Wana huruma ya Kristo kwa ajili ya wengine na wako tayari kuwasaidia wengine. Kol 3:12-14; 2 Kor 9:7; Efe 4: 11-14.
Somo hili litaendelea…


Jumatano, 11 Juni 2014


UANAFUNZI (DISCIPLESHIP)

2 Tim 2:2 “Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine”.

Ukweli wa andiko hili ni kwamba si mambo yote yanafaa kufundisha watu wote ibadani au mkutanoni. Lazima tutambue hadhira. Somo hili sio kwa ajili ya wabinafsi wanaotaka kujifunza ili tu wapone magonjwa, wabarikiwe, wainuliwe, wajulikane nk. Yaani mimi mimi mimi (me-ism). Kinyume chake ni kwa ajili ya WATU WAAMINIFU WATAKAOFAA KUWAFUNDISHA WENGINE.

I. KANUNI ZA UANAFUNZI

Mt 28:19-20 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari’.

Maneno haya yanaitwa ‘Agizo Kuu’. Biblia imejaa maagizo mengi lakini hili ni agizo kuu. Kama una shauku kuu ya moyo wa Yesu tambua kwamba agizo hapa ni ‘fanya wanafunzi’ na sio fanya washirika/washarika. Hebu tujiulize kwamba tutalifanyia kazi vipi? Hatua ya kwanza ni kuwaleta kwa Yesu na sio kuwabadilisha tu dini. Kisha lazima tuwasaidie wakue na kuwa wanafunzi wanaomjua Mungu kweli ili nao wawalete wengine kwa Yesu. Kila mkristo anatakiwa ajiwekee utaratibu angalau wa kumleta kwa Yesu mtu mmoja kwa mwaka. Swali ni je tangu umpokee Yesu una miaka mingapi, na wangapi umewaleta kwa Yesu na kuhakikisha wanakua na kuweza pia kuwaleta wengine kwa Yesu?

Tumepewa kazi muhimu ya kuwasaidia waamini wengine wakue Efe 4:11-12 ‘Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe. Tukijua kweli ya Neno la Mungu, tunawekwa huru. Yn 8:32 ‘Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru’. Yesu ndiye ukweli huo. Yn 14:6 ‘Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi’. Mtoto mchanga haachwi peke yake ajilishe.  Akiachwa peke yake atakufa. Ni kosa kubwa kuzaa watoto hospitalini na kutojali kuwapeleka mahali pa kupata malezi yanayoendana na umri wao.
Kwa nini kukua kiroho ni muhimu? Ebr 5:14 ‘Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya’. Tunakua ili tuweze kubeba majukumu makubwa. Umebeba majukumu gani makubwa ili tuseme umekua kiroho? Kama bado kuna mtu umeshindwa kumsamehe, hutoi zaka, humleti mtu kwa Yesu, unachelewa ibada kila wakati, hujishughulishi na huduma yoyote kanisani; unastahili mafundisho ya watoto wachanga. 1 Petro 2:2 Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu.

1.Uanafunzi ni nini?

Uanafunzi ni mkristo mmoja kumsaidia mkristo mwingine kukua kiroho na kukua katika uhusiano wake na Yesu Kristo.

Uanafunzi ni sawa na stuli ya miguu mitatu. Miguu hiyo ni maombi, uhusiano namafundisho. Hakuna usalama kama mguu mmoja ni dhaifu.

a)   Maombi. Yesu anasema kwamba pasipo Yeye hatuwezi kufanya lolote. Yn 15:5  ‘Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote’. Lazima tutumie muda wa kutosha katika maombi tukitafuta msaada wa Mungu na kuombea waamini wapya. Tujifunze kuweka tumaini letu kwa Mungu kuliko kwenye dini au kwa wanadamu.

b)  Uhusiano. Waamini wapya wanahitaji upendo na urafiki. Wanahitaji mfano mwema wa kuufuata. Fil 3:17 Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi’. Lazima maisha yetu yawaonyeshe kile Mungu anachotarajia. Paulo alimwonyesha Timotheo jinsi ya kuishi. Tunahitaji kujifurahisha pamoja nao, kufanya kazi pamoja, kutembea pamoja, kucheka pamoja na kulia pamoja. 2 Tim 3:10,11 ‘Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu, na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote’.


c)   Mafundisho. Waamini wapya wanahitaji mafundisho. Sehemu mojawapo katika ‘Agizo Kuu’ ni mafundisho. Wakristo wapya hawawezi kukua bila mafundisho yenye uzima. Mt 28:20 ‘na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari’.

2.Mwanafunzi ni nani?

Mwanafunzi ni mtu anayejifunza zaidi kwa Bwana wake na anayependa kufuata nyayo za Bwana wake na kubadilika akifanana naye. Mwanafunzi ni mtu anayejifunzaanayefuatana anayekua. Rum 12:2 ‘Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu’. Mwanafunzi wa kweli anatafuta kufanana na Yesu kuliko kufanana na dunia. Hebu jiulize kama uvaaji wako, mahusiano yako, matumizi yako na mapato yako yanaakisi (reflect) tabia ya Yesu Kristo.

Kanisa la kianafunzi ni kanisa ambalo linawaleta watu kwa Yesu Kristo, na kuwajenga katika imani yao na kuwaandaa wawalete wengine kwa Yesu na kuwajenga katika imani yao. Tusijali sana namba ya waumini tu wakati kati yao hakuna wanafunzi. Watumishi wa kipindi cha Biblia walitofautisha kati ya wanafunzi na makutano ya watu.

MAJINA NA TAFRI YAKE. KUNA NGUVU YA AJABU NDANI YA MAJINA HAYA


1. ELOHIM
Mwanzo 1:1, Zaburi 19:1 
Maana yake “Mungu” inarejea nguvu za Mungu na utukufu. 


2. ADONAI
Malaki 1:6
Maana yake “Bwana” inarejea ukuu wa Mungu. 


3. JEHOVAH--YAHWEH.....Mwanzo 2:4
Ina rejea wokovu mtakatifu wa Mungu.


4. JEHOVAH-MACCADDESHEM
Kutoka 31:13
Maana yake "Bwana wa kutakasa " 


5. JEHOVAH-ROHI
Zaburi 23:1
Maana yake “bwana ndiye mchungaji wangu”


6. JEHOVAH-SHAMMAH
Ezekieli 48:35
Maana yake "Mungu aliye yupo" 


7. JEHOVAH-RAPHA
Kutoka15:26
Maana yake "Bwana mponyaji wetu" 


8. JEHOVAH-TSIDKENU
Jeremia 23:6
Maana yake "Bwana wa haki" 


9. JEHOVAH-JIREH
Mwanzo 22:13-14
Maana yake "Bwana atatupa" 


10. JEHOVAH-NISSI
Kutoka 17:15
Maana yake "Bwana ni ishara yetu"

NILIMPENDA MSICHANA KUMBE NI JINI NA AMENITESA SANA


Naitwa Patrick Bundala niko mailimoja Kibaha ni mwajiriwa wa serikali ni Askari ila nyumbani ni Tabora na huku niko kikazi tu, nina mke na watoto 4. Kuna kitu kibaya kilinitokea nikiwa kozi ya uongozi huko Zanzibar mwaka 2009, tukiwa kozi tulikua tunapata mapumziko siku za weekend hivyo kutumia nafasi hiyo kwenda kutembea beach na siku hiyo ya tukio baya  ilikua jumamosi ambapo tuliondoka tukiwa wengi tu kama 50 na kwenda maeneo ya kilimani karibu na migombani ambako kuna beach nzuri sana na siku ya jumamosi jioni beach huwa inajaa watu wa kila aina na siku hiyo haikua mara ya kwanza mimi kwenda huko beach kwani kila weekend lazima niende huko beach ili kuburudisha macho na kuangalia mazingira na watu maana mimi kwa Zanzibar ilikua mara ya kwanza kwenda hivyo kwa umaarufu wa Zanzibar nilitaka hadi natoka huko niwe na cha kuwasimulia huku nyumbani kumbe ilikua bahati mbaya sana kwangu siku hiyo, wakati siku hiyo tumefika beach tulitawanyika kila mtu eneo analotaka na wengine walienda kuogelea na mimi licha ya kufahamu kuogelea lakini siku hiyo sikutaka kuogelea lakini nilitaka kutafuta binti mzuri ili nimtongoze na tuwe wapenzi na nilienda pembeni kidogo eneo ambalo watu walikua wachache na kukaa mkao wa kuangalia watu na baada kama ya dakika 40 alipita dada mmoja aliyevaa ninja akiwa ni nusu mwaarabu na nusu mwafrika na nikajikuta namtamani sana alinipita kidogo na kugeuka na kuniangalia na mimi nikaona hiyo ndio nafasi ya kumwogelesha na kikamwita akaja na ajabu sikumwambia chochote lakini sijui aligundua kuwa natafuta mwanamke maana alisogea na kunisalimia na akakaa pembeni yangu na kunichangamkia sana, na kwa sababu nilitaka mpenzi nilidhani kuwa huyo ni changudoa ambaye huwa anaenda kutafuta wanaume beach, Baada ya kukaa tuliendelea na story na ajabu yule dada akaniambia mwenyewe kuwa amenipenda sana maana nimemjali na mimi nikaona kuwa  hiyo nafasi ya kumpata mrembo yule siwezi kuipoteza na muda huo huo nikaanza kumwambia mambo ya mapenzi maana nilidhani ni kahaba na nilipomwambia hivyo alicheka na kusema amekubali ila anataka ajue kwanza jina langu, kwa sababu ya kuepusha maswali ya kuulizwa zaidi na ili asije akakataa kwa sababu ya majina yangu ya kikristo japokua hata kanisani sijawahi kwenda nilimwambia kuwa mimi naitwa Saleh Juma na yeye akasema anaitwa Munira, akafurahi sana na kusema kuwa nafaa sana na amefurahi sana kukutana na mimi. Sikutaka kuopoteza nafasi hiyo nilimwambia kuwa tunaweza kuwa wote usiku ule? akasema mbona mapema sana nikasema kwa sababu amenivutia sana, akaongea kwa madaha na kusema amekubali na kwa sababu ya binti yule nilisahau yote na kumwambia tuondoke twende tukaongelee guest house akakubali na tukaondoka saa ile ilie na kupanda gari za airport na tukashukia mkunazini na kutafuta gest tulipata na nikaalipia na tukaingia chumbani na lengo langu japokua nililipia chumba hadi asubuhi lakini nilitaka tu tufanye mapenzi na niondoke kuwahi foleni ya usiku kule kozi, tukiwa chumbani tulianza michezo ya kimapenzi na akanivulisha nguo zote na mimi nikamvulisha nguo zote isipokua nguo ya ndani na baadae kidogo akashuka kitandani na kusimama huku akinitazama kwa macho makali sana nikaanza kushtuka na ghafla kibanio chake cha nywele kikaachia ghafla na tukio la ajabu sana likatokea nywele zake zikalefuka na kuongezeka zikajaa chumba chote, nikiwa nimejilaza kitandani nilikaa ghafla na baada ya muda kidogo zile nywele zilisinyaa na kuwa za kawaida na kile kibanio kijiweka mahali pake na kubana nywele, Munira akasema kuwa yeye ni jini na anataka tu damu yangu kwani ana njaa sana nilikimbilia mlangoni ghafla huku nikiwa uchi na kujaribu kufungua mlango lakini haukufunguka japokua hatukufunga, akasema siwezi kumtoroka hata siku moja na kwa sababu mimi nimempenda na yeye amependa nyama yangu na damu yangu, nilijikaza lakini nilikua hoi karibu na kuzimia na nikaona njia iliyobaki ni kupiga kele ili watu waje kunisaidia na nilipopiga kele sauti haikwenda kokote maana nilipanua mdogo kwa nguvu zangu zote lakini sauti iliyotoka ni kama namng'ong'eza mtu kiukweli nikikua kama nimechanganyikiwa na niliposhidwa zoezi hilo niliwaza kuwa njia iliyobaki ni kulibembeleza tu lile jini na nilipoliangalia nilikuta linakwato miguuni na miguu ina manyoya kama mbuzi na meno limetoa na kuwa marefu zaidi ya rula ya kupigia mistari, Hakuwa tena yule msichana mrembo munira ambaye nilimpenda sana kwa muda mfupi, Nilimwambia yule jini anibadilishie adhabu akakataa na nilijikuta naomba maombi kwa MUNGU anihurumie na ajabu kama dakika 5 zilizofuata mlango uligogwa na ghafla lile jini likawa Munira yule wa beach na kwa sababu ya mlango kuendelea kugongwa yule jini alienda kufungua na mimi muda huo nikaanza kuvaa nguo kiaskari yaani nusu dakika nimeshavaa zote, Alikua ni dada wa mapokezi akileta chakula chipsi mayai na  na soda na munira kwa ujanja akasimama katikati ya mlango na kuanza kusema sisi hatukuagiza chochote na muda huo huo nikwamwambia yule dada aingie ndani maana kuna kitu nataka kumtuma akaja na alipokaribia tu nikatoka ghafla na kumwaga kile chakula chote huku nikisema kuwa yule dada sio mtu ni jini yule dada mhudumu naye akaakimbia na sikujua kilichoendelea ila nadhani yule jini alipotea muda huohuo maana nilipofika tu nje nilimkuta akinisubiri na kuniambia sina ujanja wa kumtoroka na kwasababu ilikua ni barabarani na watu wengi wanapita nilipiga kelele na kusema jamani niokoeni na vijana fulani waliokua wanapita mmoja wao akasema wewe umekua chizi yaani unaongea peke yako niliondoka kwa kukimbia kama mita 100  na kupanda gari ambayo ilinipekeka hado kambini na nilipofika tu kambini nilimwona tena yule jini na akaniambia kuwa kuniua lazima anaiue tu tena usiku uleule nilipiga tena kele na askari wenzangu wakaanza kucheka sana wakisema nimepandisha mashetani na nikawaelezea kuwa sijapandisha chochote ila ni hali halisi na nikawasimulia mwanzo wa tukio hadi mwisho na usiku huo sikulala maana usiku wa saa 7 nilimwona tena yule munira jini na nikapiga kelele na wenzangu kwa hasira wakasema nisiwasumbue lakini mmoja wao ambaye ameokoka akaniambia namhitaji YESU ili niwe huru. Kwa sababu ya shida nilimwambia niko tayari kuokoka kuanzia sekunde ile, akasema kuwa wao wana kundi lao la maombi hapo kozi ambalo ni kundi la waliookoka kutoka makanisa mbalimbali na huwa wana ratiba ya maombi hivyo muda ukifika atanijurisha ili twende wote na muda huo akaniombea ulinzi wa MUNGU. Muda wa maombi ulipofika tulikwenda na niliombewa na wakati wa maombezi ikasikika sauti kuwa ipo siku watanipata tu. lakini namshukuru MUNGU sana maana nilipona tangu saa ile na nimeendelea na wokovu hadi leo na hakuna chochote walichofanya. Nampenda YESU na namshukuru sana kwa kuniponya na kuniokoka pia kuniepusha na mabaya yale. MUNGU akubariki sana ndugu mtumishi wa MUNGU.

Monday, October 6, 2014

UNGANISHA SADAKA YAKO NA UWEPO WA MUNGU ILI AJIDHIHIRISHE KWAKO


by Mwl. Christopher Mwakasege - Day 1
(Viwanja vya Reli - Arusha 9/09/2012)
LENGO: Kuimarisha uhusiano wako wewe na MUNGU kwa kusaidia namna ya kuunganisha sadaka yako, na uwepo wa MUNGU Ipasavyo.
Mambo matatu yanayohusha uwepo wa MUNGU
1. Kunatofauti ya uwepo wa MUNGU na unafanya kazi na ule uwepo wa MUNGU uliopo lakini haufanyi kazi.
Luka 5:17 “Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na uyahudi, na Yerusalemu; na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya”
Utaona namba uwepo wa MUNGU ulikuwa mahali hapo,
1 Samweli 4:1-22
2. Ukitoa Sadaka palipo na uwepo wa MUNGU uliokazini(Active)/unaofanya kazi utajua
**Mwanzo 4:3-16 “Hapa tunaona kwa habari ya Kaini na Habili walipotoa sadaka na kwavile kulikuwa na uwepo wa MUNGU mahali pale Mungu alikubali sadaka ya Habili na kukataa ya Kaini, lakini siyo tu alikataa sadaka ya Kaini bali alimkataa pia na Kaini mwenyewe, Hivyo uwepo wa MUNGU ukiwepo Active utajua tu…
**Matendo 4:36 hadi Matendo 5:1-4 “Hapa utapata habari za Anania na Safina walipo jaribu kumdanganya roho wa MUNGU, mahali pale kulikuwa na uwepo wa MUNGU sasa kilichofanya uwepo wa MUNGU kujifunua nikuweka yaliyowazi maana Anania na Safina walidhani watamdanganya Petro, na kumbe kulikuwa na Uwepo wa Bwana mahali pale…
3. Ukitoa Sadaka Mahali palipo na Uwepo wa MUNGU na usijizihirishe unamaana kuna namna unatakiwa ufanye ili kusukuma/kuwasha/kufanya utukufu wa Bwana uwe Active..
**1 Samwel 1:1-6,9 “Hapa tunamwona Ana ambaye yeye alikuwa hana mtoto, Analichukua uamuzi wa kuingia madhabahuni na kufanya au kuwasha uwepo wa MUNGU uwe active, ni kweli Ana alikuwa anakwenda madhabahuni na alikuwa anatoa sadaka, lakini ilibidi atafute namna ya kuweka Uwepo wa MUNGU uwe active, ndipo anaalimwekea MUNGU nadhiri, na kumbuka NADHIRI ni sadaka yako ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako, sawasawa na kitabu cha Kumbukumbu la Torati 23:23
2 Wafalme 4:8-17 “Tunamwona mwanamke ambaye hakuwa na mtoto na alijua inabidi ataufute namna yakuwesha Uwepo wa MUNGU kuwa active, nikweli alikuwa anaomba sasa ilibidi amwambie mumewe watengeneze chumba na tena waweke na kitanda ili mtumishi wa MUNGU apate kulala, najua siyo jambo la kawaida maana hata hajawahi kulala na tena ukifikiria je kama hasingekuja na mwanamke huyo hana mtoto? Kwahiyo yeye alichojali nikutafuta uwepo wa MUNGU kwani sadaka yake ni kumtuza mtumishi wa MUNGU,(Gehazi)
UNGANISHA SADAKA YAKO NA UWEPO WA MUNGU IPASAVYO
by Mwl. Christopher Mwakasege - Day 2
(Viwanja vya Reli - Arusha 10/09/2012)
LENGO: Kuimarisha uhusiano wako wewe na MUNGU kwa kusaidia namna ya kuunganisha sadaka yako, na uwepo wa MUNGU Ipasavyo.
Umuhimu wa Imani katika kumuunganisha mtoa sadaka na MUNGU
Waebrania 11:1 “Basi Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyooneka”.
Imani inamambo Mawili(2)
*Wakika wa mambo yatarajiwayo
*Wakika ndani
Imani inakupa kuona yale yasiyoonekana/usiyoyaona(Fursa ya mambo usio yaona) au inakupa kupita ambako watu wengine wanaona hapapitiki
Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neon la Kristo”.
Mastari wa 10 “Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata hakim, na kwa kinywa ukiri hata kupata wokovu”.
Imani haitakiwi iende peke yake ni lazima iende na kitu, na kitu moja wapo ni matendo. “Imani pasipo matendo imekufa”
Unapotoa sadaka ni lazima uunganishe na imani, kwani imani ndio Connector.
Mfano: Waebrania 11:1-33 Inazunumza juu ya Imani na Matendo watu waliyofanya Imani(Waliofanyia imani kazi)
Kwenye Mstari wa 4-31 Wametajwa watu 11 waliotumia imani…
*Tuangalie watu 5 katika hoa 11
Mstari wa 4 “Kwa Imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali akinena”
Mstari wa 17-19 “Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; nay eye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee;18 naam, yeye aliyeambiwa , katika Isaka uzao wako utaitwa, 19 akihesabu ya kuwa Mungu awza kumfufua hata kutoka kuzimu; akampata tena toka huko kwa mfano”.
Habari ya Isaka utaona habari ya sadaka ya mtoto sasa kile chakula ilikuwa sadaka ya
Kunatofauti katika kumpa mzazi sadaka na kumsaidia, na Baraka zake ni tofauti pia.
Mstari 28 utaona jinsi mussa alivyotoa sadaka maana biblia iansema kwa Imani akaifanya Pasaka, sasa uwe na uwakika Pasaka ni uzaliwa wa kwanz…
Mstari wa 31 “Kwa Imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani.
• Katika watu hawa 5 Mungu alimpa mwalimu kufanya Asilimia kulinganisha na wale wote 11, Mwalimu alipata asilimia 45.5% sasa unaweza ona toka Asilimia 100% kwa nini katika sadaka?
Watu hawa walivyotoa sadaka walifungua ukurasa mpya wa maisha yao, MUNGU aliwapatia ukurasa mpya
Mungu akiachilia ukurasa mpya watu wakitoa sadaka, kama watu wakiipoteza hawataipata tena.
Rahabu asingetoa sadaka kwa imani(huku na uwepo wa MUNGU ufanyao kazi) asigne toka katika eneo hilo(ukahaba)
Imani ni Connector ya Future
Mwanzo 15:1-21
Baada ya hayo “maana yake urudi nyuma kabla ya hayo”
Baada ya sadaka mambo hayo(ya awali)
Mungu alimuuliza Ibrahimu kuhusu future baada ya kutoa sadaka ya Fungu la Kumi
Mstari wa 7 “Kisha akamwambia, Mimi ni BWANA, niliyekueta kutoka Uru wa Wakaidayo nikupe nchi hii ili uirithi”
Mstari wa 8 “Akasema, Ee Bwana MUNGU, nipateje kujua ya kwamba nitairithi?
Kinacho msumbua Ibrahimu ni kutokuwa na mtoto ndo maana alipata ujasili wa namna atakavyo rithi nchi..
Mungu alimjibu amatie ndama wa miaka 3, maana yake Mungu alitaka sadaka maana ni taratibu kutoa sadaka
Siyo Sadaka tu Ibrahimu aliachia ni lazima uwe na uwakika na Imani(Uwepo wa MUNGU) ilikuwepo, maana kila mtu anaweza kutoa sadaka
Maswali yatakayo kusaidia kukuza Imani katika hili
1. Mungu anaptaka utoe sadaka, anataka nini kwako?(MUNGU anapata nini?)
2. Wewe utapta nini?(MUNGU atakupa nini?)
3. Nisipotoa anachotaka na unachotaka kitatokea nini? (Ni kikauka kutoa utapata nini?
4. Nimekaribia kiasi gain sura mpya ya maisha yangu ili niweze kutoa sadaka?