Vichwa vya Habari

SOMO LA IMANI



SOMO: IMANI (1)
Imani maana yake nini? (Waebrania Mlango 11)
1 Basi IMANI NI KUWA NA HAKIKA ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana. 
• Ni hakika ya mambo yanayongojewa kudhihirika, ni hakika ya mambo ambayo hayajadhihirika bado; kwamba yatadhihirika.
• Neno hakika ina maana ya kwamba NI KUYAONA KUWA NI MAMBO HALISI YALE YALIYOKUWEPO, YALIYOPO SASA, NA YALE YATAKAYOKUWEPO-KUWA NI HALISI SASA! mambo yale yasiyoonekana ndivyo yalivyo HALISI SASA, bila badiliko lolote. – Na hii ndiyo tofauti ya imani, na elimu nyingine, kama sayansi!
2 Maana kwa hiyo wazee wetu walishuhudiwa.
• IMANI SI KUJILAZIMISHA- Hivyo, kutenda kwa imani ni lazima UONE USHUHUDA; NI LAZIMA USHUHUDIWE MOYONI MWAKO! Pasipo shaka yoyote ile.
NI USHUHUDA MBAO UNAKUPA UFAHAMU WA NDANI MOYONI MWAKO.
• Ufahamu huo ni wa ndani, yaani hisia za ndani katika 
o KUONA UHALISI PICHA YA KIIMANI, 
o KUSIKIA KWA DHAHIRI MOYONI MWAKO SAUTI YA IMANI, 
o KUGUSA KIHALISI KWA MGUSO WA IMANI, 
o KUONJA LADHA KWA IMANI, 
o KUPATA HARUFU KWA IMANI, 
o Katika yale yaliyokuwepo, yaliyopo, na yatakayokuwepo, kuwa ni dhahiri sasa, japo hauyaoni, hauyagusi, hauyaonji, hausikii harufu, wala hausikii sauti – KWA JINSI YA UFAHAMU WA NJE (WA MWILINI). 
• HIVYO MATOKEO YAKE 
(1) KUYAPOKEA KIUHALISI NA KUYAMILIKI 
(2) AU KUYAPOKEA KIHALISI KWA AJILI YA KUTOA NA KUMPA MWINGINE 
(3) KUWA NA UJASIRI KWA KUWA MUNGU AMESEMA NA WEWE-ATATIMIZA KWA KUWA YEYE NI MUAMINIFU HAWEZI KUSEMA UONGO. 
(4) KUPATA TUMAINI 
(5) KUWA NA NGUVU YA SABURI – KUVUMILIA NA KUDUMU KATIKA KUMNGOJA BWANA.
(6) KUWA NA MSIMAMO PASIPO KUYUMBISHWA NA CHOCHOTE KILE!
(7) KUMFURAHIA, KUMSIFU, KUMUINUA, KUMTUKUZA, NA KUMSHANGILIA MUNGU; PAMOJA NA KUZISHANGILIA AHADI ZAKE KUU ZA NENO LAKE ASEMALO!
3 Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri. 
4 Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali akinena. 
5 Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu. 
6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao. 
7 Kwa imani Nuhu akiisha kuonywa na Mungu katika habari za mambo yasiyoonekana bado, kwa jinsi alivyomcha Mungu, aliunda safina, apate kuokoa nyumba yake. Na hivyo akauhukumu makosa ulimwengu, akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani. 
8 Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. 
9 Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake(yaani, alipata picha halisi ya imani ya umiliki wa nchi ya ahadi), akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. 
10 Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu. 
11 Kwa imani hata Sara mwenyewe alipokea uwezo wa kuwa na mimbaI(yaani, alipata mguso wa halisi wa imani); alipokuwa amepita wakati wake; kwa kuwa alimhesabu yeye aliyeahidi kuwa mwaminifu. 
12 Na kwa ajili ya hayo wakazaliwa na mtu mmoja, naye alikuwa kama mfu, watu wengi kama nyota za mbinguni wingi wao, na kama mchanga ulio ufuoni, usioweza kuhesabika. 
13 Hawa wote wakafa katika imani, wasijazipokea zile ahadi, bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia, na kukiri kwamba walikuwa wageni, na wasafiri juu ya nchi. 
14 Maana hao wasemao maneno kama hayo waonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe. 
15 Na kama wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea. 
16 Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana amewatengenezea mji. 
17 Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee; 
18 naam, yeye aliyeambiwa, Katika Isaka uzao wako utaitwa, 
19 akihesabu ya kuwa Mungu aweza kumfufua hata kutoka kuzimu; akampata tena toka huko kwa mfano. 
20 Kwa imani Isaka akawabariki Yakobo na Esau, hata katika habari ya mambo yatakayokuwa baadaye. 
21 Kwa imani Yakobo, alipokuwa katika kufa, akambariki kila mmoja wa wana wa Yusufu, akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake. 
22 Kwa imani Yusufu, alipokuwa amekaribia mwisho wake, alitaja habari za kutoka kwao wana wa Israeli, akaagiza kwa habari ya mifupa yake. 
23 Kwa imani Musa, alipozaliwa, akafichwa miezi mitatu na wazazi wake, kwa sababu waliona kwamba ni mtoto mzuri; wala hawakuiogopa amri ya mfalme. 
24 Kwa imani Musa alipokuwa mtu mzima, akakataa kuitwa mwana wa binti Farao; 
25 akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo; 
26 akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo. 
27 Kwa imani akatoka Misri, asiogope ghadhabu ya mfalme; maana alistahimili kama amwonaye yeye asiyeonekana. 
28 Kwa imani akaifanya Pasaka, na kule kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wao. 
29 Kwa imani wakapita kati ya Bahari ya Shamu, kama katika nchi kavu; Wamisri walipojaribu kufanya vivyo wakatoswa. 
30 Kwa imani kuta za Yeriko zikaanguka, zilipokwisha kuzungukwa siku saba. 
31 Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani. 
32 Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii; 
33 ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba, 
34 walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni. 
35 Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora; 
36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani; 
37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya; 
38 (watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi. 
39 Na watu hao wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi; 
40 kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ili wao wasikamilishwe pasipo sisi

No comments:

Post a Comment

NENO NI UZIMA Designed by 5gear Copyright © 2014-2015

Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.