Vichwa vya Habari

Kwa Nini Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?


Kwa Nini Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?

Jibu la Biblia

Mungu hakuwa na mke halisi ambaye walipata naye watoto. Lakini ndiye Muumba wa vitu vyote. (Ufunuo 4:11) Kwa hiyo, Adamu, mwanadamu wa kwanza ambaye Mungu alimuumba, anaitwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Vilevile, Biblia inafundisha kwamba Yesu aliumbwa na Mungu. Hivyo, Yesu pia anaitwa “Mwana wa Mungu.”—Yohana 1:49.
Mungu alimuumba Yesu kabla ya kumuumba Adamu. Kumhusu Yesu, Mtume Paulo aliandika: “Yeye ndiye mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.” (Wakolosai 1:15) Maisha ya Yesu yalianza miaka mingi kabla ya kuzaliwa katika zizi huko Bethlehemu. Hata Biblia inasema kwamba “asili yake ni kutoka nyakati za kale, kutoka siku za wakati usio na kipimo.” (Mika 5:2) Kabla ya kuzaliwa akiwa mwanadamu hapa duniani Yesu, Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu, alikuwa kiumbe wa roho huko mbinguni. Yesu mwenyewe alisema hivi: “Nimeshuka kutoka mbinguni.”—Yohana 6:38;8:23.

No comments:

Post a Comment

NENO NI UZIMA Designed by 5gear Copyright © 2014-2015

Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.