Vichwa vya Habari

UTIIFU WA KWELI MBELE ZA MUNGU


UTIIFU WA KWELI MBELE ZA MUNGU

Kama Abraham a

livyokuwa "rafiki Wa Mungu" kwa uvumilivu na utiifu kwa Mungu, wewe pia unaweza kumjua Mungu na kupata rehema zake, amani, na baraka. Kumjua Mungu kwa uvumilivu wa kweli katika kumwamini ni ujuzi muhimu zaidi katika maisha. Ni ajabu namna gani kwamba Mungu hujidhihirisha Mwenyewe kwa wote wanao Mtafuta kwa mioyo yao yote!

Ikiwa utageuka kuiacha njia yako na kweli kujitolea kwa Mungu, Roho Wake ataishi ndani yako. Hakuna kitakacho kutenganisha na upendo Wake unapo tumainia ahadi Zake na Kumfuata kwa utiifu. Yeye atakuwa Mungu wako, nawe utakuwa hazina Yake Mwenyewe. Utagundua kwamba alikununua kwa gharama kuu, na anataka kuwa na ushirika nawe—sasa na hata milele.

Uliza Mungu akupe ufahamu unapojifunza kurasa hizi za vifungu kutoka Neno la Mungu. Mungu aliongoza watu wamchao kuandika maneno haya na kwa kimiujiza ameyahifadhi katika vizazi vyote kutoka kwa majaribio yote ya Shetani ya kuyakomesha.
______________________________________________________________
Maandiko yanayo husika katika kijitabu hiki yametolewa kutoka Biblia: Sheria (Torah), Zaburi (Zabur), maandiko ya manabii, na Injili (Injil).


KUNA MUNGU WA KWELI MMOJA TU — 1
Kumbukumbu La Torati 6:4, 5
BWANA, Mungu wetu, BWANA ndiye mmoja. Nawe mpende BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.

Isaya 45:18
Maana BWANA, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine.
1 Wafalme 8:60
Watu wote wa ulimwengu Wajue ya kuwa BWANA ndiye Mungu; hakuna mwingine.
Mimi ni BWANA; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu. —Isaya 42:8
Isaya 43:10, 11
Ninyi ni mashahidi wangu, asema BWANA,. . . mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine. Mimi, naam, mimi, ni BWANA, zaidi yangu mimi hapana mwokozi.
Isaya 45:22
Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.

MUNGU NI WA REHEMA NA NEEMA — 2
Zaburi 103:8, 11
BWANA amejaa huruma na neema, haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili. Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, kadiri ileile rehema zake ni kuu kwa Wamchao.
Zaburi 103:17, 18
Bali fadhili za BWANA zina Wamchao tangu milele hata milele,...maana, wale walishikao agano lake, na kuyakumbuka maagizo yake ili wayafanye.
Mika 7:18
Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu,...kwa maana yeye hufurahia rehema.
Maombolezo 3:22
Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, kwa kuwa rehema zake hazikomi.
Maombolezo 3:32
Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.
Zaburi 18:25
Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili.
1 Mambo Ya Nyakati 16:34
Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele.

MUNGU ANAKUPENDA — 3
Yeremia 31:3
BWANA alinitokea zamani, akisema, Naam, nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
Yeremia 29:11
Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani, wala Si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.
Malaki 1:2
Nimewapenda ninyi, asema
 BWANA.
Zaburi 103:13
Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, ndivyo BWANA anavyowahurumia wamchao.
Isaya 38:17
Tazama; nalikuwa na uchungu mwingi kwa ajili ya amani yangu; Lakini kwa kunipenda [ee Mungu] umeniokoa na shimo la uharibifu; kwa maana umezitupa dhambi zangu zote nyuma yako.
1 Yohana 4:16, 19
Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.
Sefania 3:17
BWANA, Mungu wako, yu katikati yako shujaa awezaye kuokoa; atakushangilia kwa furaha kuu, atatulia katika upendo wake. Atakufurahia kwa kuimba.

JAMBO KUBWA MUHIMU MAISHANI NI KUMJUA MUNGU — 4
Danieli 11:32
Lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu.
Yeremia 9:24
Bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, ya kuwa mimi ni BWANA, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema BWANA.
Kumbukumbu La Torati 30:19, 20
Nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, kumpenda BWANA, Mungu wako, kuitii sauti yake na kushikamana naye: kwani hiyo ndiyo uzima wako.
Zaburi 119:2
Heri wazitiio shuhuda zake, wamtafutao kwa moyo wote.
Zaburi 42:1
Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji. Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu.
Kutoka 33:14
Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.

KUJITEGEMEA PASIPO MUNGU NI KUANGAMIA — 5
2 Mambo Ya Nyakati 15:2
BWANA yu pamoja nanyi, mkiwa pamoja naye; nanyi mkimtafuta ataonekana kwenu; lakini mkimwacha atawaacha ninyi.
Yeremia 17:9
Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?
Mithali 16:25
Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; lakini mwisho wake ni njia za mauti.
2 Petro 2:4, 9
Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu. Basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu.
1 Samweli 12:15
Bali msipoisikia sauti ya BWANA, mkiiasi amri ya BWANA, ndipo mkono wa BWANA utakuwa juu yenu.
Yohana 15:6
Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatu. pa motoni yakateketea.

KUMJUA MUNGU NI LAZIMA TUMTAFUTE — 6
Yeremia 29:13
Nanyi mtanitafuta, na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.
Mithali 2:4, 5
Ukiutafuta kama fedha, . . . ndipo utakapo . . . pata kumjua Mungu.

Mathayo 7:7
Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.
Waebrania 11:6
Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba
 huwapa thawabu wale wamtafutao.
Mithali 8:17
Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Maombolezo 3:25
BWANA ni mwema kwa hao wamngojeao, kwa hiyo nafsi imtafutayo.
Matendo 17:26, 27
Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja. ...Ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.

MUNGU ANATUTAKA TWENDE KWAKE — 7
2 Mambo Ya Nyakati 30:9
Kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye mwenye neema, na mwenye rehema, wala hatawageuzia mbali uso wake, mkimrudia.
Zaburi 86:5
Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema, umekuwa tayari kusamehe, na mwingi wa fadhili, kwa watu wote wakuitao.
Yakobo 4:8
Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.
Zaburi 145:18
BWANA yu karibu na wote Wamwitao, wote wamwitao kwa uaminifu.
Isaya 1:18
Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.
Mathayo 11:28, 29
Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu.
Yohana 6:37
Wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe.

MUNGU NI MTAKATIFU — 8
Kutoka 15:11
. . . Ni nani aliye kama wewe, Ee BWANA, . . . mtukufu katika utakatifu.
1 Samweli 2:2
Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA; kwa maana hakuna ye yote ila wewe.
Ayubu 34:10
Mungu asidhaniwe kutenda udhalimu; wala Mwenyezi kuf anya uovu.
Isaya 6:3
Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni BWANA wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake.
Isaya 57:15
Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu.
Zaburi 145:17
BWANA ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.
Marko 10:18
Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.
Ufunuo 15:4
Ni nani asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu.

WATU WA MUNGU NI LAZIMA WAISHI MAISHA MATAKATIFU — 9
Yakobo 2:19, 20
Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka. Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai?
1 Yohana 2:4; 3:10
Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake. Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; bali humpenda mtu afuatiaye wema. —Mithali 15:9
Waebrania 12:14
Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao.
Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote. —1 Petro 1:15
Amosi 5:14
Tafuteni mema, wala si mabaya, mpate kuishi; hivyo BWANA, Mungu wa majeshi, atakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo.

MAMBO MUNGU ANAYOAMURU — 10
Mika 6:8
Na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!
Mambo Ya Walawi 19:2
Mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi BWANA, Mungu wenu, ni mtakatifu.
Luka 10:27
Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.
Marko 10:19
Wazijua amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usi danganye, Waheshimu baba yako na mama yako.
Warumi 12:2
Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu.
Yoshua 1:8
Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.
Marko 11:22
Mwaminini Mungu.

MAMBO MUNGU ANAYOCHUKIA — 11
Mithali 6:16-19
Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA; naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; moyo uwazao mawazo mabaya; miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu; shahidi wa uongo asemaye uongo; naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.
Isaya 61:8
Maana mimi, BWANA, naipenda hukumu ya haki, nauchukia wivi na uovu.
Ufunuo 21:8
Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.
Malaki 2:15, 16
Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. Maana mimi nakuchukia kuachana, asema BWANA.
Zekaria 8:17
Wala mtu wa kwenu asiwaze mabaya moyoni mwake juu ya jirani yake; wala msipende kiapo cha uongo; maana hayo yote ndiyo niyachukiayo, asema BWANA.

WATU HUPUNGUKIWA NA MATAKWA YA MUNGU — 12
Walakini nimewajua ninyi ya kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu. —Yohana 5:42
Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. —Yakobo 2:10
Isaya 6:5
Ndipo niliposema, Ole wangu! kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, BWANA wa majeshi.
Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi. —Yakobo 4:17
Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, hakuna mwenye haki hata mmoja. —Warumi 3:10
Warumi 3:23
Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
1 Yohana 3:10
Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
Isaya 53:6
Sisi sote kama kondoo tumepotea; kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe.
Ni nani awezaye kusimama mbele za BWANA, huyu Mungu mtakatifu? —1 Samweli 6:20

KAZI ZETU WENYEWE HAZIWEZI KUMPENDEZA MUNGU — 13
Warumi 10:2, 3
Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.
Isaya 64:6
Kwa maana sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu, na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa unajisi.
Ezekieli 33:13
Nimwambiapo mwenye haki, ya kwamba hakika ataishi; kama
 akiitumainia haki yake, akatenda uovu, basi katika matendo yake ya haki, hata mojawapo halitakumbukwa; bali katika uovu wake alioutenda, atakufa katika uovu huo.
Warumi 8:8; 3:20
Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu. Kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria.
2 Wakorintho 3:5
Si kwamba twatosha sisi wenyewe kufikiri neno lo lote kwamba ni letu wenyewe, bali utoshelevu wetu watoka kwa Mungu.

DHAMBI HUTUTENGANISHA NA MUNGU — 14
Warumi 5:12
Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.
Yakobo 1:15
Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.
Ezekieli 18:20
Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa.
Isaya 59:2
Lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na
 dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.
Mithali 11:19
Haki huelekea uzima; afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.
2 Mambo Ya Nyakati 24:20
Mungu asema hivi, Kwani ninyi kuzihalifu amri za BWANA, hata msiweze kufanikiwa? Kwa kuwa mmemwacha BWANA, yeye naye amewaacha ninyi.
1 Samweli 15:23
Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, yeye naye amekukataa wewe.

GHADHABU YA MUNGU JUU YA DHAMBI — 15
Zaburi 7:11
Mungu ni mwamuzi mwenye haki, naam, Mungu aghadhibikaye kila siku.
Nahumu 1:3
BWANA si mwepesi wa hasira, ana uweza mwingi, wala hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe.
Wakolosai 3:6
Kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu.
Warumi 1:18
Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.
Warumi 1:29-32
Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.

HUKUMU IKO MBELE — 16
Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu. Waebrania 9:27
Ufunuo 20:12, 15
Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.
Waebrania 10:31
Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.
Mathayo 12:36
Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la sir likiwa jema au likiwa baya. —Mhubiri 12:14
Mathayo 13:49, 50
Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki, na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

HATUWEZI KUJIFICHA KUTOKANA NA MUNGU — 17
Mithali 15:3
Macho ya BWANA yako kila mahali; yakimchunguza mbaya na mwema.
Zaburi 139:1-4
Ee BWANA, umenichunguza na kunijua. Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu; umelifahamu wazo langu tokea mbali. Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, umeelewa na njia zangu zote. Maana hamna neno ulimini mwangu usilolijua kabisa, BWANA.
1 Samweli 16:7
Kwakuwa BWANA haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali BWANA huutazama moyo.
Zaburi 94:9
Aliyelitia sikio mahali pake asisikie? Aliyelifanya jicho asione?
Yeremia 16:17
Maana macho yangu yaziangalia njia zao zote; hawakufichwa uso wangu usiwaone, wala haukusitirika uovu wao macho yangu yasiuone.
Waebrania 4:13
Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.

KUGEUKA NA KUTOKA DHAMBINI KUNAHITAJIKA — 18
Ezekieli 18:23
Je! mimi ninafurahia kufa kwake mtu mwovu? asema Bwana MUNGU; si afadhali kwamba aghairi, na kuiacha njia yake, akaishi?
Luka 13:3
Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.
Mithali 28:13
Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.
Yoeli 2:12, 13
Lakini hata sasa, asema BWANA, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea; rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema.
Hosea 14:2
Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie BWANA; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema.
Ayubu 33:27, 28
Yeye huimba mbele ya watu, na kusema, mimi nimefanya dhambi, yeye ameikomboa nafsi yangu isiende shimoni, an uhai wangu utautazama mwanga.

KUTUBU KUNALETA MSAMAHA — 19
Isaya 55:6, 7
Mtafuteni BWANA, maadamu
 anapatikana, mwiteni, maadamu yu karibu; mtu mbaya na aache njia yake, na mtu asiye haki aache mawazo yake; na amrudie BWANA, naye atamrehemu; na arejee kwa Mungu wetu, naye atamsamehe kabisa.
Zaburi 34:18
BWANA yu karibu nao waliovunjika moyo, na waliopondeka roho huwaokoa.
Yeremia 36:3
Wapate kurudi, kila mtu akaiache njia yake mbaya; nami nikawasamehe. . . dhambi yao.
Zaburi 32:5
Nalikujulisha dhambi yangu, wala sikuuficha upotovu wangu. Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA, nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.
1 Yohana 1:9
Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.
Matendo 3:19
Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe.
Kutubu kunamaanisha kugeuka kutoka dhambini pamoja na kuungama mbele za Mungu.

DHABIHU INAYOTAKIKANA KUTUPATANISHA NA MUNGU — 20
(Dhambi ilileta utengano.)
Mambo Ya Walawi 17:11
Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi.

Waebrania 9:22
Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo

Kutoka 12:5, 13
Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka mmoja. ...
Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu yenu, lisiwapate pigo lo lote likawaharibu.

Mwanzo 22:8, 13
Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-kondoo kwa hiyo sadaka, mwanangu. . . . Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.

YESU NDIYE MWANA KONDOO ALIYETOLEWA NA MUNGU — 21
Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu! —Yohana 1:29
Alionewa, lakini alinyenyekea, wala hakufunua kinywa chake; kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, na kama vile kondoo anyamazavyo mbele yao wakatao manyoya yake; naam, hakufunua kinywa chake. —Isaya 53:7
Wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele. Kadhalika Kristo naye, akiisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi. . . . Basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai? —Waebrania 9:12,28, 14

1 Petro 1:18, 19
Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.

UKOMBOZI NI KWA MAAFIKANO TU NA MUNGU — 22

Warumi 3:24, 25
Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake.
Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. —Warumi 5:8,9
Hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu. —Wagalatia 2:16
Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. —Waefeso 2:8,9
Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi. —Matendo 10:43

Matendo 4:12
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.

KUZALIWA KWA YESU KWATANGAZWA — 23

Luka 1:26-38
...
Malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. ...Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, ...na ufalme wake utakuwa hauna mwisho. Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.... kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu. Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.
Watu tu walioingia Ulimwenguni pasipo uzao wa Mume na Mke walikuwa Adamu na Kristo. Adamu alileta dhambi katika Ulimwengu, lakini Yesu alileta ushindi juu ya dhambi.

KWA KWELI YESU NI NANI — 24

Wafilipi 2:6, 8
Ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

Yohana 10:30, 36
Mimi na Baba tu umoja. Je! yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?
Yesu Kristo, Neno la Milele, amekuwako daima. Kwa muujiza, Mungu alisababisha atungwe mimba katika tumbo la Mariamu. Kimwili anajulikana kama Mwana wa Mtu, na Kiroho anajulikana kama Mwana wa Mungu. Maandiko yanatumia neno "Mwana" kueleza uhusiano ulioko kati ya Mungu na Neno lake—Yesu Kristo.

Waebrania 10:5
Kwa hiyo ajapo . . . Lakini mwili uliniwekea tayari.
Na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu. —Warumi 1:4

Yohane 20:28
Tomaso akajibu, akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu!

KWA KWELI YESU NI NANI — 25

1 Timotheo 3:16
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili.

Wakolosai 2:9
Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.

Isaya 9:6
Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.

Yohana 8:58
Yesu akawaambia, . . . Yeye
 Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukum tambua. —Yohana 1:10

1 Timotheo 2:5, 6
Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote.

Wakolosai 1:14, 15
Ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi; naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana.

BIBLIA (MAANDIKO) NI NENO LA MUNGU — 26
Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. —2 Petro 1:21

Luka 1:70, 77
Kama alivyosema tangu mwanzo kwa kinywa cha manabii wake watakatifu; uwajulishe watu wake wokovu, katika kusamehewa dhambi zao.
Roho ya BWANA ilinena ndani yangu, na neno lake likawa ulimini mwangu. —2 Samweli 23:2
Kumbukumbu La Torati 6:6
Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako.

2 Timotheo 3:16
Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki.

Warumi 15:4
Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini.

Mathayo 22:29
Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.

Zaburi 138:2
Kwa maana umeikuza ahadi yako, kuliko jina lako lote.

YESU NDIYE NENO LA MUNGU — 27

Ufunuo 19:13
Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

Yohana 1:1, 14
Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu.

Yesu anamdhihirisha Mungu
2 Wakorintho 4:6
Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang’aa toka gizani, ndiye aliyeng’aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo.

Yohana 1:18
Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.
Mungu yuanena kuptia kwa Yesu
Waebrania 1:1, 2
Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.

Yohana 8:38
Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo.

NENO LILILOANDIKWA NA LILILO NA UHAI KU LINGAN ISHWA — 28,29

Biblia ni chakula kwa nafsi
Ayubu 23:12
Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu.

Mathayo 4:4
Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

Biblia inaangaza njia yetu
Zaburi 119:105
Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.
Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, na kumfahamisha mjinga. —Zaburi 119:130
Yesu ni mkate kutoka mbinguni
Yohana 6:51, 48
Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. Mimi ndimi chakula cha uzima.
Yesu ni nuru ya ulimwengu
Yohana 8:12
Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
Biblia huleta maisha yen ye mazao
Zaburi 1:2, 3
Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, na sheria yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti uliopandwa kandokando ya vijito vya maji, uzaao matunda yake kwa majira yake, wala jani lake halinyauki; na kila alitendalo litafanikiwa.
Yesu hutoa maisha yen ye mazao
Yohana 15:4a, 5
Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi; akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.
MAANDIKO YAELEZA JUU YA YESU KRISTO
Yohana 5:39, 46
Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. . . . Kwa maana kama mngalimwamini Musa, mngeniamini mimi; kwa sababu yeye aliandika habari zangu.

Luka 24:27
Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.

NENO LA MUNGU LA MILELE HALIBADILIKI — 30
Zaburi 119:89, 160
Ee BWANA, neno lako lasimama imara mbinguni hata milele. Jumla ya neno lako ni kweli, na kila hukumu ya haki yako ni ya milele.

Isaya 40:8
Majani yakauka, ua lanyauka; bali neno la Mungu wetu litasimama milele.

Mathayo 5:18
Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie.

Yohana 10:35
Na maandiko hayawezi kutanguka.
Mtu asijaribu kubadilisha maneno ya Biblia
Kumbukumbu La Torati 12:32
Neno niwaagizalo lo lote liangalieni kulifanya; usiliongeze, wala usilipunguze.

Mithali 30:6
Usiongeze neno katika maneno yake; asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.
Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima. —Ufunuo 22:19
Mithali 13:13a
Kila alidharauye neno hujiletea uharibifu.

KIFO CHA YESU KILIKAMILISHA MPANGO WA MUNGU — 31

Yohana 10:17, 18
Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena.
Mathayo 26:53, 54
Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika? Yatatimizwaje basi maandiko, ya kwamba hivyo ndivyo vilivyopasa kujiri?

Matendo 3:18
Lakini mambo yale aliyohubiri
 Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo.

Matendo 2:23
Mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua.

Isaya 53:10
Lakini BWANA aliridhika kumchubua; amemhuzunisha; utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi.

KIFO CHA YESU KUTANGAZWA NA MASHAHIDI — 32
Marko 15:27, 28
Na pamoja naye walisulibisha wanyang’anyi wawili, mmoja mkono wake wa kuume na mmoja mkono wake wa kushoto. Basi andiko likatimizwa linenalo, Alihesabiwa pamoja na waasi.
Mathayo 27:45, 50-51, 54
Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa. . . . Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. . . . nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka. Basi yule akida, na hao waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu, walipoliona tetemeko la nchi na mambo ya
 liyofanyika, wakaogopa sana, wakisema, Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.
Yohana 19:32-37
Basi askari wakaenda, wakamvunja miguu wa kwanza, na wa pili, aliyesulibiwa pamoja naye. Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu; lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji. ...Kwa maana hayo yalitukia ili andiko litimie, hapana mfupa wake utakaovunjwa. Na...watamtazama yeye waliyemchoma.

YESU ALISHINDA KIFO — 33

Matendo 2:24, 32
Ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao. Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.
Waebrania 2:14, 15
Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi, awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa.

1 Wakorintho 15:55, 57
Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako? Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Ufunuo 1:18
Na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.
2 Timotheo 1:10
Na sasa inadhihirishwa kwa kufunuliwa kwake Mwokozi wetu Kristo Yesu; aliyebatili mauti, na kuufunua uzima na kutokuharibika, kwa ile Injili.

YATUPASA TUFANYEJE NA YESU? — 34

Ufunuo 3:20
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauWa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki. —Warumi 4:5
Yohana 20:22; 16:24
Pokeeni Roho Mtakatifu...ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.

Warumi 10:9
Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni
 Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.
Mathayo 10:37, 16:24, 25
Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; ...Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.
Wagalatia 3:29
Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.

KUPITIA KWA YESU TUNA UZIMA MPYA — 35

1 Yohana 5:11, 12
Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.
Wagalatia 2:20
Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu.

Warumi 8:2
Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu
 imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.

2 Wakorintho 5:17
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! yamekuwa mapya.
1 Petro 1:23; 2:2
Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele. Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu.

MUNGU NI BABA KWA WATU WAKE — 36

Zaburi 68:5
Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane, Mungu katika kao lake takatifu.
Isaya 64:8, 63:16
Lakini sasa, Ee BWANA, wewe u baba yetu; sisi tu udongo, nawe u mfinyanzi wetu; sisi sote tu kazi ya mikono yako. Wewe, BWANA, ndiwe Baba yetu, mkombozi wetu tangu milele ndilo jina lako.

Hosea 1:10
Tena itakuwa, badala ya kuambiwa, Ninyi si watu wangu, wataambiwa, Ninyi ndio wana wa Mungu aliye hai.

Mathayo 7:11; 6:9
Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?. . . Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje.

2 Wakorintho 6:17b, 18
Nami nitawakaribisha. Nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike.
Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu. —Warumi 8:14

KUPITIA KWA YESU TUNAMJUA MUNGU KAMA BABA — 37

Yohana 14:6, 7, 23
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona. Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.
Wagalatia 4:4-7; 3:26
...Mungu alimtuma Mwanawe...
ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana. Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu ali mtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba. Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu. Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.

Yohana 1:12
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.

1 Yohana 2:1
Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki.

YESU HULETA UPENDO, FURAHA, AMANI — 38

1 Yohana 4:16
Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

Waefeso 4:32
Tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi. —Yohana 13:35
Wagalatia 5:22
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani...
Walakini nitamfurahia BWANA, nitamshangilia Mungu wa wokovu wangu. —Habakuki 3:18

Zaburi 16:11
Utanijulisha njia ya uzima; mbele za uso wako ziko furaha tele; na katika mkono wako wa kuume mna mema ya milele.

Warumi 5:1
Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na tuwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Yohana 14:27
Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.

YESU ATAWAFUFUA WAFUASI WAKE WA KWELI — 39

Warumi 8:11
Lakini, ikiwa Roho wake yeye
 aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu.
1 Wakorintho 6:14
Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa uweza wake.
Yohana 11:25, 26
Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele.
1 Wakorintho 15:21-23
Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa. Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja.

Yohana 14:19
Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.

USIDHARAU WOKOVU HUU MKUU — 40

Waebrania 10:28, 29
Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu. Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?

Yohana 12:48
Yeye anikataaye mimi, asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumuye; neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho.
Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakuf a katika dhambi zenu. —Yohana 8:24

Luka 12:4, 5
Nami nawaambia ninyi rafiki zangu, msiwaogope hao wauuao mwili, kisha baada ya hayo hawana wawezalo kutenda zaidi. Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumwua mtu ana uweza wa kumtupa katika Jehanum; naam, nawaambia, Mwogopeni huyo.

Waebrania 2:3
Sisi je! tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii?

YESU KRISTO ATATUHUKUMU — 41

Matendo 17:31
Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu.

Yohana 5:22, 23
Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, bali amempa Mwana hukumu yote; ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba.

2 Wakorintho 5:10
Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee. kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya.

Warumi 2:16
Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, kwa Kristo Yesu.

2 Wathesalonike 1:7, 8
Wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake; katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu.

Luka 19:27
Tena, wale adui zangu, wasiotaka niwatawale, waleteni hapa mwachinje mbele yangu.

SIO WOTE WANAOSHUHUDIA KUMFUATA YESU WALIO WA YESU — 42

Tito 1:16
Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana.

Warumi 8:9
Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.

Ezekieli 33:31
Nao hukaa mbele yako kama watu wangu, nao husikia maneno yako, wasiyatende; maana kwa vinywa vyao hujifanya kuwa wenye upendo mwingi, lakini mioyo yao inatafuta faida yao.

Mathayo 15:8
Watu hawa huniheshimu kwa midomo; ila mioyo yao iko mbali nami.

Mathayo 7:21-23
Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika uf alme wa mbinguni; bali ni yeye af anyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

WAFUASI HALISI WA YESU HUMII — 43

1 Yohana 2:3
Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake.

Ezekieli 36:27
Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda.

Waebrania 5:9
Naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii.

Warumi 6:18
Na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki.

Waefeso 2:10
Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

Warumi 8:10, 13
Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki. Kwa maana kama mkiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.

2 Timotheo 2:19
Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu.

ULIMWENGU UNACHUKIA WAFUASI WA YESU — 44

Yohana 15:18, 19
Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi. Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake, lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.

Yohana 16:2, 3
Naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.

1 Yohana 3:1
Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.

Matendo 14:22
Na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.

2 Timotheo 3:12
Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.

Yohana 16:33
Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.

AHADI KWA WANAO DHULUMIWA — 45
Huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. —1 Petro 5:7

Isaya 41:10
Usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
Baba yangu na mama yangu wameniacha, bali BWANA atanikaribisha kwake. —Zaburi 27:10

Waebrania 13:6
Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?

1 Petro 4:14
Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.

Zaburi 91:11; 23:4
Kwa kuwa atakuagizia malaika zake wakulinde katika njia zako zote. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya; kwa maana Wewe upo pamoja nami.
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu. Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu. —Wafilipi 4:13, 19

USHINDI JUU YA DHAMBI NA SHETANI — 46

1 Wakorintho 10:13
Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

Waebrania 4:16
Basi na tukikaribie kiti cha flee-ma kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.

2 Timotheo 2:22
Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.

1 Yohana 1:7
Bali tukienenda nuruni, kama yeye ahivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.

Warumi 6:11
Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.

Yakobo 4:7
Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.

Zaburi 119:11
Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, nisije nikakutenda dhambi.

MAOMBI YA KWELI NI USHIRIKA NA MUNGU — 47

Zaburi 27:8
Uliposema, Nitafuteni uso Wangu, Moyo wangu umekuambia, BWANA, uso wako nitautafuta.

Zaburi 62:8
Enyi watu, mtumainini sikuzote, ifunueni mioyo yenu mbele zake; Mungu ndiye kimbilio letu.

Yeremia 17:14
Uniponye, Ee BWANA, nami nitaponyeka; uniokoe, nami nitaokoka; kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu.

1 Wathesalonike 5:17, 18
Ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.
Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa. —Yakobo 1:5
Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa. —Yohana 15:7

Zaburi 34:4
Nalimtafuta BWANA akanijibu, akaniponya na hofu zangu zote.

Zaburi 66:18; 25:11
Kama ningaliwaza maovu moyoni mwangu, Bwana asingesikia. Ee BWANA, kwa ajili ya jina lako, unisamehe uovu wangu, maana ni mwingi.

YESU ANAKUJA—UWE TAYARI! — 48

1 Wathesalonike 4:16, 17
Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi, farijianeni kwa maneno hayo.

2 Wakorintho 7:1
Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.

1 Yohana 2:28
Na sasa, watoto wadogo, kaeni ndani yake, ili kusudi, atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake katika kuja kwake.

Yakobo 5:8, 9
Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia. Ndugu, msinung’unikiane msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.

Luka 12:40
Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu.

UJAZWE NA ROHO WA MUNGU
Mithali 1:23
Geukeni kwa ajili ya maonyo yangu; tazama, nitawamwagia roho yangu, na kuwajulisheni maneno yangu.

Matendo 2:38
Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Waefeso 5:18-21
Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho; mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo; hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo.

Wafilipi 2:13
Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.

1 Wakorintho 3:16; 6:2
Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? Maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.

Text from Bible in Kiswahili, United Bible Societies, Africa Regional Centre, ©1952. Used by permission.
If you are interested in receiving additional studies of God’s Word, write to the publisher or order online:
W.M. Press, Inc.
P.O. Box 120
New Paris, Indiana 46553 U.S.A.
Bure — Hakiuzwi
1515 Kiswahili

NENO NI UZIMA Designed by 5gear Copyright © 2014-2015

Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.