Vichwa vya Habari

Nafsi Ni Nini?







Nafsi Ni Nini?


Jibu la Biblia

Katika Biblia, neno “nafsi” limetafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebraniane′phesh na neno la Kigiriki psy·khe′. Katika Kiebrania neno hilo kihalisi linamaanisha “kiumbe kinachopumua,” na katika Kigiriki linamaanisha “kiumbe kilicho hai.” * Kwa hiyo, nafsi ni kiumbe chenyewe, si kitu fulani kilicho ndani ya mtu ambacho huendelea kuishi mwili unapokufa. Hebu ona jinsi Biblia inavyoonyesha kwamba nafsi ya mwanadamu ni mwanadamu mwenyewe:





Adamu alipoumbwa akawa nafsi hai





Adamu hakupewa nafsi—yeye mwenyewe “akawa nafsi hai”
  • Yehova Mungu alipomuumba mwanadamu wa kwanza, Adamu, Biblia inasema kwamba “mtu akawa nafsi hai.” (Mwanzo 2:7,Union Version) Adamuhakupewa nafsi—yeye mwenyewe alikuwa nafsi, yaani, mtu mwenyewe.
  • Biblia inafundisha kwamba nafsi inaweza kufanya kazi, inaweza kutamani chakula, inaweza kula, inaweza kutii sheria, na hata kugusa mzoga. (Mambo ya Walawi 5:2; 7:20; 23:30;Kumbukumbu la Torati 12:20;Waroma 13:1) Bila shaka, mambo hayo hufanywa na mtu mwenyewe kwa ujumla.

Je, nafsi inaweza kufa?

Ndiyo, nafsi inaweza kufa. Maandiko kadhaa katika Biblia hutaja waziwazi kwamba nafsi inaweza kufa. Ona baadhi ya maandiko hayo:
  • “Nafsi inayofanya zambi, itakufa.”Ezekieli 18:4, 20Zaire Swahili Bible.
  • Katika taifa la kale la Israeli, mtu alipofanya moja kati ya yale makosa mazito zaidi, mara nyingi sheria ilisema “nafsi hiyo atakatiliwa mbali.” (Kutoka 12:15, 19Union VersionMambo ya Walawi 7:20, 21, 27; 19:8) Mtu huyo “lazima auawe.”Kutoka 31:14Biblia Habari Njema.
  • Maandiko mengine ya Biblia yanapozungumzia kuhusu mtu aliyekufa yanatumia maneno “nafsi . . . iliyokufa.” (Mambo ya Walawi 21:11;Hesabu 6:6) Ingawa tafsiri nyingi za Biblia zinatumia neno “maitikatika mistari hiyo, Kiebrania cha awali, kinatumia neno ne′phesh,au “nafsi.”

Neno “nafsi” linaweza kutumiwa pia kumaanisha “uhai”

Pia, Biblia hutumia neno “nafsi” na “uhai” kumaanisha kitu kilekile. Kwa mfano, Ayubu 33:22 (Union Version) linatumia neno la Kiebrania la “nafsi” (ne′phesh) kumaanisha “uhai.” Biblia inaonyesha kwamba nafsi au uhai unaweza kuhatarishwa au hata kupotezwa.Kutoka 4:19;Waamuzi 9:17; Wafilipi 2:30.
Kutumia neno “nafsi” kwa njia hiyo kunatusaidia kuelewa mistari ya Biblia inayoirejelea nafsi kuwa ‘inatoka.’ (Mwanzo 35:18) Usemi huo wa mfano unaonyesha kwamba mtu yuko karibu kufa. Katika andiko hilo laMwanzo 35:18 tafsiri nyingine za Biblia zinatumia maneno “alipopumua pumzi yake ya mwisho.”Neno—Biblia Takatifu.

Imani ya kwamba nafsi haifi ilitoka wapi?

Makanisa ya Kikristo yanayofundisha kwamba nafsi haifi yalirithi fundisho hilo, si kutoka katika Biblia, bali kutoka kwa falsafa za kale za Wagiriki. Kitabu Encyclopædia Britannica kinasema: “Biblia inaporejezea kuhusu nafsi inahusianisha nafsi na wazo la pumzi na kamwe haisemi kwamba nafsi na mwili ni vitu viwili tofauti, eti kwamba kuna nafsi ya ulimwengu wa roho na mwili wa ulimwengu huu. Mafundisho ya dini za Kikristo kwamba mwili na nafsi ni vitu viwili tofauti yalitokana na Wagiriki wa kale.”
Mungu haungi mkono hata kidogo wazo la kupatanisha mafundisho yake na falsafa za wanadamu, kama vile imani ya kwamba wanadamu wana nafsi isiyoweza kufa. Anatoa onyo hili katika Biblia: “Mjihadhari: labda kuna mtu ambaye atawachukua ninyi kama windo lake kupitia falsafa na udanganyifu mtupu kulingana na pokeo la wanadamu.”Wakolosai 2:8.

No comments:

Post a Comment

NENO NI UZIMA Designed by 5gear Copyright © 2014-2015

Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.