Vichwa vya Habari

SIFA ZA UPENDO WA KIUNGU (AGAPE)



BWANA YESU Asifiwe ndugu msomaji, leo tupitie somo kuhusu Upendo wa Kiungu (AGAPE) na sifa zake. 2WAKORINTHO 13:1-13.
Upendo wa Kiungu ni hali ya kupenda mtu bila kujali mtu huyo alivyo au ana sifa gani.
*Mtu aliye na Upendo huu huchukuliana na kila mtu pasipo kujali tabia yake au sifa zake.
*Mtu aliyeokoka na kujazwa Roho Mtakatifu anao Upendo huu.
*Upendo ni Sifa na Amri kuu ya mtu aliyeokoka.
*Huu ni Upendo wa kipekee tofauti na Upendo wa kidunia tunaoufahamu ambao mtu hupendwa kutokana na jinsi alivyo, pesa zake,mali zake, umaarufu wake, cheo chake, n.k. Upendo huu ni zaidi ya hapo.
- Tukumbuke kuwa sisi sote tulikuwa wenye dhambi na wenye uchafu wa kila aina lakini Upendo huu Alionao Mungu Baba, haukujali hayo yote tuliyokuwa nayo, bali Yeye Alilipa gharama ya kumtoa Mwanawe wa Pekee, Yesu Kristo, Mungu Mtakatifu, Akajitoa sadaka kwa ajili Yetu wenye dhambi. YOHANA 3:16
- Hii inatufundisha jambo la kipekee sisi tuliopokea Upendo huo, basi nasi tuudhihirishe kwa wale wasiomjua Kristo, ili wavutwe waokoke.
SIFA ZA UPENDO WA KIUNGU (AGAPE)
*Upendo huvumilia
*Hufadhili
*Hauhusudu
*Hautakabari
*Haujivuni
*Haukosi kuwa na adabu
*Hautafuti mambo yake
*Hauoni uchungu
*Hauhesabu mabaya
*Haufurahii udhalimu
*Hufurahi pamoja na kweli
*Huvumilia yote
*Huamini yote
*Hutumaini yote
*Hustahimili yote
*Haupungui neno wakati wowote
>Hizi ni sifa za kipekee ambazo twahitaji kumwomba Roho Mtakatifu Atuwezeshe kuwa nazo ili tuweze kufika Mbinguni.
1PETRO 4:8 'Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi'
MUNGU AKUBARIKI SANA!

No comments:

Post a Comment

NENO NI UZIMA Designed by 5gear Copyright © 2014-2015

Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.