Vichwa vya Habari

SIKU ZA MWISHO BWANA YESU ATARUDI ATACHUKUA WALIO WAKE






















Mojawapo ya jambo ambalo halijawahi kuzoeleka na wala halitazoeleka, ni kifo. Kifo amekuwa adui mkubwa mno wa mwanadamu. Ingawa wakati mwingine mwanadamu apatwapo na mambo magumu sana hutamani kifo, lakini ukweli ni kwamba bado ni jambo lisilozoeleka.
Hakika ndugu unayesoma ujumbe huu kama hujawaho kufiwa na wazazi wako, basi umefiwa na kaka, dada ama wadogo zako. Kama katika hayo yote bado, basi umefiwa na rafiki yako mliyependana sana. Kama hamna, basi umefiwa na mke, mme au mchumba wako mliyetarajia kuoana. Hakika kwa kila namna sote tumeumizwa na kifo. Hivyo kifo ndo maana hakijawahi kuzoeleka.
Lakini hivi kweli kifo kitaacha kutuua au kutuulia jamaa zetu lini? Mara nyingi maswali magumu yasiyo na majibu huulizwa na wafiwa, "Nitampata wapi mtu mwingine kama huyu?" "Mbona afe huyu na wala si wengine, hivi MUNGU nimemkosea nini mimi?" Kama watu hao wakikosa majibu katika maswali yao magumu, hujiingiza katika mambo mabaya kama kunywa pombe, kuvuta bangi na kula madawa ya kulevya wakifikiri kwamba huenda vitu hivyo vitatuliza huzuni zao kuu.
Lakini sisi wafanya kazi wa ukurasa huu wa "Matukio Ya Mwisho Wa Dunia" kwa nguvu za MUNGU Atupendae tunakuleteeni habari za Matumaini;
"Ndugu zenu wote walio kufa mtawaona tena"
Habari hii ni ya uhakika wala si ya mashaka. Twatamani mkumbuke kwamba haya matukio magumu yanayotokea duniani ni ishara ya dunia kutetemeka kwa sababu kuna Mmoja Anakuja akiwa na mng'aro wa kama mwanga wa jua mara bilions. Huyo ni YESU KRISTO Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana na Rais wa marais. Huyo ndiye Anayekuja kukomesha kifo maana Yeye ni kiboko ya kifo kwa sababu kifo kilijaribu kummeza lakini baada ya siku tatu hakukiweza kuendelea kumshikiria kwa vile Yeye ni Shujaa. Na Alipokuwa akitoka kaburini alituthibitishia kuwa anao tayari ufunguo wa kifo hivyo Atakaporudi kifo ni kukiangamiza kifo kabisa. KRISTO Atafuta machozi yetu huku akitupa pole kwa kujibu maswali yetu magumu tuliyohoji juu ya kifo.
Mpendwa, pamoja na kwamba ujumbe wetu wa leo umekuwa mrefu kiasi, lakini tunapenda tumalizie kwa kusema kwamba; Hatuna budi kusisitiza ndugu, kaka, dada, mjomba, shangazi, bibi na jamaa zetu wengine kumwamini huyu YESU Ajaye ili akisha kuja tupate kufurahia sote kwa kuishi milele bila kifo maaana lazima tuseme ukweli huu ili watu tusije tukabweteka.
Ukweli ni kwamba wale ndugu zetu ambao hawakumwamini YESU na kufa dhambini, watafufuliwa ndiyo lakini baadae watachomwa moto na kubaki majivu tu wala kumbukumbu lao halitakuwepo kabisa.
Mfariji Wa Ajabu's photo.
Hivyo kwa vile twaamini wawapenda ndugu na jamaa zako, usiwaonee aibu kuwaasa wamwamini KRISTO ili hata wafapo, wawe na sehemu yao katika ufufuo wa kuingia maisha mapya yasiyo na machozi, mauti, maombolezo, vilio na maumivu.

No comments:

Post a Comment

NENO NI UZIMA Designed by 5gear Copyright © 2014-2015

Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.