Vichwa vya Habari

ASKOFU KAKOBE AZIDI KULITETEA NENO LA MUNGU

ASKOFU KAKOBE AZIDI KULITETEA NENO LA MUNGU


Askofu mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zakaria Kakobe hivi karibuni aliongea maneno makali kwa watumishi wa Mungu yaliyopelekea baadhi ya watu (kanisa) kujihoji kuhusu maisha yao na wakati huo huo wengi ikiwemo watumishi wa Mungu kukemea hali ya Askofu huyo kuhukumu bila kuwajua wahusika maisha yao binafsi na Mungu.

Askofu Kakobe alimwakia Rose Muhando kwa wazi  na kusema “Leo sikwepeshi…wanaume wanatikisa viuno Rose Muhando, hiyo ni team ya kwenda motoni, hakuna Mungu humo ndani….watu wanaoenda mbinguni hawako hivyo Rose Muhando rudi msalabani kama hujazaliwa mara ya pili zaliwa leo.Unatikisa viuno…..viuno unaleta kanisani,viuno peleka bar Rose Muhando kila mahali stage show, stage show, vitu hivi havikuwepo assemblies, vitu hivi havikuwepo kwa wapentekoste, nani atainuka mchungaji kukemea, kila mtu anajifanya ameokoka lakini huoni wokovu ule ”

Aliendelea kuwashukia wanasiasa maarufu kama Nape Nnauye, Mh. Mwakyembe, Mh. Lazaro Nyarandu na Paul Makonda na kuwataka  wajipime, warudi msalabani na kuzaliwa mara ya pili. Aliendelea zaidi na kusema “Mimi hapa sihitaji mtu, Waziri ukija hapa, Raisi ukija hapa utanisaidia nini, Raisi huwezi kunipa hela mimi.. mimi ndio nitakupa, mimi sihitaji hela ya mtu, Mungu aliyeniita ana fedha na dhahabu vyote ni mali yake, sihitaji hela ya mwanasiasa, sihitaji hela ya waziri…wakija kuleta harambee zao hapa watajisifu, tutashindwa kuwapiga kama hivi ninavyowapiga, lakini sasahivi ninakupiga Nape, nakupiga Makonda, Nakupiga Mangula, siangalii sura ya mtu hapa….Injili iko pale pale.Hakuishia hapo alimshukia mtumishi wa Mungu TB Joshua na kusema “Na tunaona mlolongo wa watu sasahivi wanajifichaficha wanaenda kwa TB Joshua, kwenye mchanganyo, TB Joshua hata haubiri kuhusu kuzaliwa mara ya pili, anazungumza vitu vya ajabu ajabu na miujiza feki, watu wanajazana hapo kama Mwigulu NchembaMpaka sasa hakuna Mchungaji aliyemjibu Askofu Zakaria Kakobe.

No comments:

Post a Comment

NENO NI UZIMA Designed by 5gear Copyright © 2014-2015

Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.