Vichwa vya Habari

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU - SEHEMU YA PILI

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU - SEHEMU YA PILI

I Wakorintho 14:12; ''Vivyo hivyo na ninyi kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa''.

UTENDAJI KAZI WA KARAMA.
Mambo muhimu (ya msingi) kufahamu ili karama ziweze kufanya kazi. Mambo hayo ni:-
1.) kubali kuwa karama za Roho zinaweza kufanya kazi kwako pia. I Wakorintho 12:4.11; ''Basi pana tofauti za karama bali Roho ni yeye yule, lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye''. Roho Mtakatifu ndani ya mtu anazo karama zote bali anamgawia kila mtu kama apendavyo yeye. Rumi 12:3-6; inasema ''kwa maana kwa neema niliyopewa na mwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyo mpasa kunia ..........., basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali ..............''.




2.) Uwe na hamu (haja) kubwa ya msaada wa Mungu. I Wakorintho:1,12; ''ufuateni upendo na kutaka sana karama za rohoni, lakini zaidi kwamba mpate kuhutubu, vivyo hivyo na ninyi kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa''.
Angalizo: karama siku zote zina mvuto.
3.) Tembea katika wito (nafasi) yako. Warumi 12:6, ''......... kwa kadri ya neema tuliyopewa...'', yaani wito (kiwango) ulichopewa. Ndani ya wito kuwa nafasi ambayo Mungu amekupa. Kuna ngazi, kuna mahali na muda unaotakiwa kuufanyia huo wito. Galatia 2:6-7 ''......walipokwisha kujua neema niliyopewa........ walinipa mimi mkono wa kuume wa shirika''.
Mfano: kuna tofauti ya karama ya unabii na huduma ya unabii, yaani kila mtu aliyeokoka anaweza kutoa unabii bali si kila mtu ana karama ya unabii.
4.) karama kutenda kazi vizuri ndani ya mtu inategemea kiwango cha Imani alichonacho. Rumi 12:6; ''basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali ........ ikiwa unabii tutoe unabii kwa kadri ya imani''. Sio zaidi ya hapo. Rumi 10:17; ''imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neno la kristo'' yaani kiwango cha imani ulichonacho hakiwezi kuzidi hapo. Imani huja tu kwa neno la Kristo. Biblia haituruhusu kutembea kwenye karama zaidi ya imani tuliyo nayo.
Angalizo: kufahamu neno la Kristo kwa wingi ni muhimu. Tembea katika karama za roho kwa kadri ya imani.

Jambo la nne linaendelea:
Karama zitumike kwa kadri ya Imani yaani utendaji kazi wa karama za Roho Mtakatifu ndani ya mtu utategemea kiwango cha neno la kristo kilichoko ndani yake. Hii ni kwa sababu Mungu alikusudia kuwa karama katikati ya kanisa zifanye kazi kwa ufanisi na usalama ili kulijenga kanisa.
Mfano: Mungu hakuweka unabii ili uongoze kanisa; ila ni kwa ajili ya kuthibitisha neno ambalo Mungu amekwisha kulisema ndani ya mtu.
Kwa sababu karama si zako ni za Roho Mtakatifu, kama huna neno la kutosha ndani yako karama inaweza ikaletwa ndani yako ukaikataa.
I Wakorintho 12:8 ''maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa apendavyo Roho yeye yule''. I Petro 4:10; ''kila mmoja kwa kadri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana....''. Kuna kupewa na kupokea- karama. Unaweza kukataa kwa kutokuja au hofu n.k.
5.) Jifunze jinsi Roho anavyowasiliana na roho yako, nafsi yako na mwili wako. I Wakorintho 3:16; ''hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?'' Mtu ni roho anayo nafsi na anaishi katika mwili. Roho Mtakatifu pia yuko ndani ya mwili. Hesabu 30:2 ''Mtu atakapo mwekea Bwana nadhiri, ....... Asitangue neno lake; atafanya sawasawa na hayo yote yamtokayo kinywani mwake''. Unaposema maneno yanafunga nafsi yako. Mwili unatawaliwa na nafsi, nafsi kazi yake ni kutafsiri kile ambacho mwili unasema ili roho ielewe na kile ambacho roho inasema ili mwili uelewe. Kwa hiyo nafsi inasaidiwa pale, unaposoma neno ili iweze kutafsiri mambo ya rohoni sawasawa na neno. Marko 2:5-8, ''naye Yesu, alipoiona imani yao, ........ wakifikiri mioyoni mwao ..... Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao .....''. Galatia 6:17; ''tangu sasa mtu asinitaabishe kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.

6.) Ujazo wa Roho Mtakatifu. Sio wa siku moja ambao unatosheleza. I Petro 4:9-11 ''mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung'unika, kila mmoja kwa kadri alivyoipokea karama,........... mtu akihudumu na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu, .......''. yaani kila wakati kuna nguvu fresh, mtu asihudumu kwa nguvu alizojaliwa bali anazojaliwa kila wakati na Mungu. Hivyo tunahitaji kurudi kwa Mungu kila wakati kujazwa nguvu za Roho Mtakatifu.
Kuna kiwango cha nguvu za Roho Mtakatifu ndani ya mtu ambacho hakiwezi (kwa kuwa ni kidogo) kusukuma karama fulani ili ziweze kuhudumu au kufanya kazi; ndio maana tunahitaji kujazwa kila wakati.

No comments:

Post a Comment

NENO NI UZIMA Designed by 5gear Copyright © 2014-2015

Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.