Vichwa vya Habari

YESU akasema ‘Kaeni Katika Neno Langu’

‘Kaeni Katika Neno Langu’
“Mkikaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, nanyi mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.”—YOHANA 8:31, 32.
Inamaanisha Nini? “Neno” la Yesu linamaanisha mafundisho yake, ambayo chanzo chake ni cha juu zaidi. Yesu alisema: “Baba mwenyeYohana 12:49) Alipokuwa akisali kwa Baba yake wa mbinguni, Yehova Mungu, Yesu alisema: “Neno lako ni kweli.” Alinukuu Neno la Mungu mara nyingi ili kuunga mkono mafundisho yake. (Yohana 17:17; Mathayo 4:4, 7,10) Kwa hiyo, Wakristo wa kweli, ‘wanakaa katika neno lake,’ yaani, wanakubali Neno la Mungu Biblia, kuwa “kweli” na msingi pekee wa imani na matendo yao.
we aliyenituma amenipa amri kuhusu jambo la kutangaza na la kusema.” (
Wakristo wa Mapema Walifanyaje Hivyo? Mtume Paulo, ambaye ndiye Mkristo aliyeandika vitabu vingi zaidi katika Biblia, aliliheshimu Neno la Mungu kama Yesu alivyofanya. Aliandika hivi: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida.” (2 Timotheo 3:16) Wanaume waliowekwa rasmi ili kuwafundisha Wakristo wenzao walipaswa “kushikamana na Neno la Mungu lililo hakika na lenye kutegemeka.” (Tito 1:7, 9The Amplified Bible) Wakristo wa mapema walihimizwa wakatae “falsafa na udanganyifu mtupu kulingana na pokeo la wanadamu, kulingana na mambo ya msingi ya ulimwengu na si kulingana na Kristo.”—Wakolosai 2:8.
Ni Nani Wanaofanya Hivyo Leo? Katiba ya Vatikani inayoitwa Dogmatic Constitution on Divine Revelation, iliyoanza kutumika mwaka wa 1965 na ambayo imenukuliwa katika kitabu kimoja cha kanisa Katoliki (Catechism of the Catholic Church) inasema hivi: “Kanisa [Katoliki] halifuati tu Maandiko Matakatifu katika kuhakikisha mambo yote yaliyofunuliwa. Kwa hiyo, mapokeo matakatifu na pia Maandiko Matakatifu yanapaswa kukubaliwa na kuheshimiwa kwa ushikamanifu uleule.” Makala moja katika gazeti laMaclean’s ilinukuu kasisi mmoja huko Toronto, Kanada, ambaye aliuliza: “Kwa nini tunahitaji kuongozwa na sauti ya ‘kimapinduzi’ ya miaka elfu mbili iliyopita? Tuna maoni mazuri ajabu, ambayo uzito wake hupungua nyakati zote kwa sababu tunalazimika kuyaunga mkono kwa kutumia Maandiko na maneno ya Yesu.”
Kitabu New Catholic Encyclopedia kinasema hivi kuhusu Mashahidi wa Yehova: “Wanaiona Biblia kuwa chanzo pekee cha imani na sheria zinazoongoza mwenendo wao.” Hivi karibuni, mwanamume fulani huko Kanada alimkatiza mwanamke fulani Shahidi wa Yehova alipokuwa akijitambulisha. “Ninajua wewe ni nani,” akasema mwanamume huyo huku akiinyooshea kidole Biblia ya Shahidi huyo, “kwa sababu una kitambulisho.”

No comments:

Post a Comment

NENO NI UZIMA Designed by 5gear Copyright © 2014-2015

Theme images by Jason Morrow. Powered by Blogger.